- MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Wednesday, May 23, 2012

Shabiki Arusha atwaa pikipiki ya Simba
Mwandishi wetu
SHABIKI wa timu ya soka ya Simba mkoani Arusha, Abubakar Hamisi, ameibuka kidedea katika droo ya bahati nasibu katika kampeni ya 'changia Simba' inayoendeshwa kwa ushirikiano baina ya Kampuni ya Push Mobile Media na klabu hiyo.
Katika bahati nasibu hiyo, Hamisi, ambaye ni dereva taxi, amejinyakulia zawadi ya pikipiki yenye thamani ya zaidi ya sh.milioni 3.

Meneja Kampeni wa Simba SMS, Talib Rashid kutoka kampuni ya Push Media Mobile (wa pili kulia), akichezesha bahati nasibu ambayo shabiki wa Simba kutoka mkoa wa Arusha, Abubakari Hassan alishinda piki piki yenye thamani shs Milioni. 1.8. Kulia ni Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga na wa tatu kushoto ni msimamizi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini, Bakari Maggid. (PICHA NA MPIGAPICHA WETU)
 Kwa mujibu wa Meneja Kampeni wa Simba Sms, Talib Rashid, shabiki huyo ni miongoni mwa mashabiki zaidi ya 40 wa klabu hiyo kongwe hapa nchini waliojishindia zawadi mbalimbali ikiwamo pesa taslim.
"Droo kubwa itafanyika Julai na mshindi atajinyakulia bajaji," alisema Rashid na kuongeza kuwa mashabiki wanatakiwa kuandika neno Simba na kutuma kwenda 15678 kuingia katika bahati nasibu hii.
Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga, alisema ushindi wa shabiki huyo ni uthibitisho tosha kwamba mashabiki wao wanashinda katika bahati nasibu hiyo.
"Naomba wanachama na mashabiki wetu wajitokeze kushiriki katika bahati nasibu hii kwani ni moja ya kuichangia klabu ya Simba iweze kujiendesha na kufanya vizuri zaidi ndani na nje ya Tanzania," alisema Kamwaga.
Mshindi atazawadiwa zawadi yake ndani ya wiki mbili kuanzia sasa, na kampuni ya Push Mobile Media itagharimia gharama za usafiri na kulala wakati wa kuja hapa jijini.
Alisema kuwa kwa sasa wamebakiza piki piki moja na bajaj ambazo drow yao itachezeshwa siku moja.

No comments:

Post a Comment