MASTAA WAZIDI KUMIMINIKA KUTALII TANZANIA - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Friday, March 28, 2025

MASTAA WAZIDI KUMIMINIKA KUTALII TANZANIA


NA MWANDISHI WETU

NYOTA wa Hollywood @sydney_sweeney ambaye alipata umaarufu wake kwa mara ya kwanza mnamo 2018 kwenye filamu ya “Everything Sucks” na “The Handmaid’s Tale” yupo nchini Tanzania akifurahia mapumziko @serengeti_national_park hali iliyowatamanisha mastaa wenzake kama @parishilton  na @jessicaalba na kucomment kwenye page zake. 


Muigizaji huyo mwenye wafuasi zaidi ya milioni 24 katika mtandao wake wa instagram amehusika pia katika filamu iliyoongozwa na Quentin Tarantino inayoitwa “Once Upon a Time”, huko Hollywood.


Mwaka 2024, aliigiza katika filamu ya kishujaa iliyopata umaarufu mkubwa ya “Madame Web”, na hivi karibuni akatayarisha na kuigiza katika filamu ya kutisha ya “Immaculate”.

 

Muigizaji hiyo amepost katika mitandao yake akionesha kufurahia mandhari za Serengeti ambapo mpaka sasa post hizo tayari zimeangaliwa na watu zaidi ya milioni 5 na kusambazwa zaidi na watu zaidi ya laki 2.



No comments:

Post a Comment