NA MWANDISHI WETU
UONGOZI wa Chuo cha Ufundi Stadi Veta
- Furahika, ambacho kipo Buguruni Malapa jijini Dar es Salaam, umeendelea
kuwasisitiza wazazi kutumia nafasi ya programu ya elimu bure kwa kuwapeleka
vijana wao kusoma fani mbalimbali bila malipo.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam,
Kaimu Mkuu wa Chuo hicho, Dkt David Msuya, amesema fursa hiyo ni ya kipekee,
hivyo vijana wasipoteze muda mtaani bila kuwa na shughuli ya kufanya waende
chuoni hapo kupata ujuzi, bure ili kujitengezea njia mpya ya mafanikio katika
maisha yao.
“Hiki chuo ni pekee hapa Tanzania
kinachotoa elimu bure kwa vijana na wanacholipia ni ada ya mtihani tu ambayo ni
shilingi 50,000 na lengo ni kuunga mkono juhudi ya Serikali ya Awamu ya Sita
inayoongozwa na Dkt Rais Samia Suluhu Hassan, kutimiza ndoto za vijana kupitia elimu
ya Amali,” amesema.
Pia amesema bado wanaendelea na
udahili wa wanafunzi ili wajiunge na muhula mpya kwa kozi za miezi mitatu, sita
na mwaka mmoja na baada ya hapo wengi wao watatafutiwa kazi kulingana na kozi
ambayo amechukua.
Ameweka wazi
kwamba wapo baadhi ya wasichana wanakwenda kufanya kazi za ndani nje ya nchi
kutokana na kukosa fursa nyumbani, hivyo ikiwa kijana hususan msichana
atajiunga na chuo hicho atafungua njia ya mafanikio katika maisha yake.
Dkt Msuya
ametaja kozi zinazofundishwa chuoni hapo ni ‘Nurser Teaching’ ikiwa katika
mgawanyo wa Ethics in Professionalism, Teaching methodology, Teaching Practice,
Philosophy, Psychology, Children Literature, Communication skills, Early
Childhood Education , School Management na First Aid in Schools.
‘Secretarial
Course’ ni nyingineyo ambayo inafundishwa na chuo hicho ikigawanyika katika ‘Shorthand,
Hatimkato, Office Practice, Secretarial Duty, Typing Skillls, Computer
Applicant, Business English na Communication Skillis.
Nyingine ni
Passengers Bus Services inayojumuisha Road Safety and Traffic Rules, Customer
Care and Communication Skillis, Internet and Emails, Transportation law na
First Aid.
Ameongeza
kuwa kozi nyingine ni Computer Application, Business Administration yenye vipengere
kama vile Introduction Business Management, Communication Skills, Computer Application
in Business, Principles of Accounting and bookkeeping, Entrepreneurship,
Marketing and Sales Management na Human Resource Management.
Pia amesema
kozi nyingine wanazofundisha ni Accounting and Finance iliyo katika mgawanyo wa
Introduction of Accounting, Financial Accounting, Business Mathematics na
Statistics, Computerized Accounting
System, Taxation and Revenue Management, Entrepreneurship.
Naye mdau wa
chuo hicho, Madaraka Omari ‘Bi Kauthar’ amesisitiza wazazi kupeleka vijana wao
katika chuo hicho ambacho ni mkombozi kwa vijana wa kitanzania ambao
wanachangamoto ya kuendelea na masomo kwa ukosefu wa ada.







No comments:
Post a Comment