TAKUKURU MKOANI PWANI YAOKOA SH. BIL 7.5 MICHANGO YA WAFANYAKAZI - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Wednesday, November 13, 2024

TAKUKURU MKOANI PWANI YAOKOA SH. BIL 7.5 MICHANGO YA WAFANYAKAZI


NA MWANDISHI WETU

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Pwani, kwa kipindi cha Julai hadi Septemba, 2024 imefanikisha ukusanyaji wa shilingi bil 1.5 kati ya bil. 7.5 ya  michango ya wafanyakazi kutoka kwa waajiri waliokuwa hawaipeleki kwenye mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

Imeelezwa kwamba kiasi hicho cha fedha ni sawa na asilimia 103 ya makusanyo ambayo yamepatikana baada ya TAKUKURU Mkoa wa Pwani kuingilia kati mfumo wa ukusanyaji michango ya watumishi kwenda mifuko ya Hifadhi ya Jamii baada ya kubaini uwapo waajiri ambao walikuwa hawapeleki michango kwa nia hovu au kwakutojua sheria.

Akizungumza leo Novemba 13, 2024 na Waandishi wa Habari mkoani Pwani, Naibu Mkuu TAKUKURU wa mkoani humo, Alli Sadiki , amefafanua kwamba sababu ya kuingialia mfumo huo ni baada ya kubaini uwepo wa waajiri 77 kwa makusudi au kwa kutofahamu sheria walishindwa kupeleka michango ya watumishi wao katika mfuko wa Hifadhi ya Jamii NSSF.

Amesema jambo hilo limewanufaisha waajiri hao na ingesababisha watumishi kushindwa kupata mafao stahiki kitu ambacho si sawa na kusababisha TAKUKURU kulifanyia kazi na wadaiwa kukubali kulipa deni la sh. 7, 505,723,317.10 kwa 20% ifikapo Julai, 2024.

Naibu Mkuu huyo wa Takukuru mkoani Pwani, amesema kwamba baada ya kufutilia na kusimamia sheria za mifuko ya Hifadhi pamoja na Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11/2007 , Julai 17, mwaka huu walifanikiwa kufanikisha makusanyo yaliyofikia Sh. 1, 543,125,427,00 yakiwa ni sawa na 103% kwenda NSSF.

 

Ameongeza kuwa kutokana na mchakato huo kufanyika waajiri hao 77, wamesema kwamba wapo tayari kushirikiana na TAKUKURU kuendeleza mapambano dhidi ya rushwa na awali changamoto hiyo ilijitokeza kwa kuwa hawakuwa na elimu ya makosa ya rushwa kwa mujibu wa Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini na Makosa ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

 

Ameibainisha kwama baadhi ya waajiri hao hawakuwa wanajua kuwa kutokupeleka michango kwa wakati NSSF ni kosa kisheria, Pia baadhi ya waajiri walikuwa hawapeleki michango kwa makusudi na kusababisha kuvunja Sheria na baada ya kupewa maelekezo walichanga bila shida.

 

“Nia ovu ya baadhi ya waajiri ilisababisha kupoteza fedha za za watumishi wao na kujinufaisha kwa kutowalipa michango NSSF na baadae ingesababisha wahusika kutopata mafao kama stahili, amesema.

Ameongeza kuwa katika kipindi hicho, pia wamefanya semina 53, mikutano ya hadhara 39, vipindi vya Redio 3, Kuimarisha Klabu za Wapinga Rushwa 53, Uandishi wa Makala 8 na TAKUKURU Rafiki 3.

 

Aidha amefafanua kuwa katika kipindi tajwa,wameendelea na utekelezaji wa Programu ya TAKUKURU Rafiki na kuzifikia jumla ya Kata Sita na kero mbalimbali zilizoibuliwa na kupatiwa ufumbuzi zikiwemo kutoka Idara ya Ruwasa, Halmashauri, Afya, TFS, Elimu na TANROADS.

 


No comments:

Post a Comment