SERIKALI YATOA MILIONI 250 UJENZI WA MADARASA KIGAMBONI - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Wednesday, March 15, 2017

SERIKALI YATOA MILIONI 250 UJENZI WA MADARASA KIGAMBONI

                                   Mbunge wa Kigamboni, Dk. Faustine Ndungulile
Suleiman Msuya

SERIKALI imetoa sh. milioni 250 zimetolewa na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa madarasa, mabweni, vyoo na maabara katika Shule ya Sekondari Nguva wilayani Kigamboni ili iweze kupokea wanafunzi wa kidato cha tano.


Hayo yamesemwa na Mbunge wa Kigamboni, Dk. Faustine Ndungulile leo jijini Dar es Salaam.
Alisema kupatikana kwa fedha hizo ni mwanzo mzuri wa kuifungua Kigamboni kielimu kwani kwa miaka mingi imekuwa haina shule ya sekondari ya kidato cha tano na sita.

“Sekondari ya Nguva iliyopo kata ya Somangila itaboreshwa na kuanza kutumika kama shule ya kidato cha tano na sita Serikali imetoa sh.milioni 250,” alisema.

Dk. Ndungulile alisema maboresho hayo yatakayoanza hivi karibuni yanatarajia kukamilika ifikapo mwezi Julai, mwaka huu.

Alisema kupatikana kwa shule ya kidato cha tano na sita, kutapanguza tatizo la wanafunzi waliofaulu kidato cha nne kwenda kusoma mbali.

No comments:

Post a Comment