RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiangalia mchele wa Mbeya wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika Marikiti Kuu ya Darajani Wilaya ya Mjini Unguja leo na kuzungumza na Mfayabishara wa Bidhaa za Vyakula katika marikiti hiyo Bw.Seif Khamis Ali na (kushoto kwa Rais) Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi na (kulia kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Idrissa Mustafa Kitwana.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na kusalimiana na Watalii wakitembelea Marikiti Kuu ya Darajani Wilaya ya Mjini Unguja, wakati wa ziara yake ya kushtukiza kutembelea Wafanyabishara ya vyakula katika Marikiti Kuu Darajani Unguja leo (Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi, wakimsikiliza Mfanyabishara wa Nyama ya Ng’ombe katika Soko la Marikiti Kuu Darajani Wilaya ya Mjini Unguja leo 18-2-2023, wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika Marikiti hiyo kuangalia hali ya bidhaa ya vyakula.(Picha na Ikulu)




No comments:
Post a Comment