
.....................................
VIONGOZI wa Shirikisho la Waendesha Bodaboda Tanzania, leo Agosti 9, 2023 wamefika katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba Dar es Salaam na kuzungumza na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Ndg. Sophia Mjema.
Viongozi hao walimuomba Ndg. Mjema kumfikishia
salamu za pongezi Mwenyekiti wa CCM, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna
anavyoongoza nchi na kutatua kero zinazowakabili wananchi wa makundi mbalimbali
wakiwemo wao.
Walimtuma Ndg. Mjema amweleze Rais Dkt. Samia
kwamba wanamuunga mkono katika kazi anazofanya kuhakikisha nchi inapata
maendeleo na maisha ya Watanzania yanakuwa bora.
Kwa upande wake Ndg. Mjema aliahidi kuzifikisha
salamu hizo na kuwashukuru kwa kuendelea kukiunga mkono Chama Cha Mapinduzi.








No comments:
Post a Comment