Mkuu wa Idara ya Usimamizi, Athari na taratibu za Benki, Peter Tarimo (katikati) akitoa taarifa za mafanikio ya benki hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2022 na kutangaza gawio kwa wanahisa wao, mchakato utakaofanyika Oktoba 6 mwaka huu.
NA MAGENDELA HAMISI
MAENDELEO BANK imetangaza gawio kwa wanahisa la Tsh. Mil 708
kwa mwaka wa fedha wa 2022 huku ikiongezeka kwa asilimia 136 tofauti na gawio
la mwaka 2011 ambalo lilikuwa sh. mil 11.
Hayo yamebainishwa leo jijini Dar es Salaam na Mkuu Idara ya
Usimamizi wa Athari na Taratibu za Benki, Peter Tarimo na kufafanua kuwa baada
ya kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa tisa wa wanahisa wamepitisha kwa pamoja mapendekezo
ya Bodi ya Wakurugenzi kwa gawio la sh. mil 26 kwa kila hisa na kufanya jumla
kufikia gawio la mil 708.
“Napenda kuchukua nafasi hii kuwafahamisha wanahisa wote
kwamba gawio lao litalipwa Oktoba 6 mwaka huu kwa wanahisa wote ambao wamo
regista ya wanahisa kwa tarehe 31Augusti 2023,” amesema.
Ameongeza kuwa ni wanne na wa pili kwa pesa taslimu tangu
kuanzishwa benki hiyo mwaka 2013 na inaonyesha dhamira yao ya kuwatunza
wanahisa kwa umiliki wao.
Amesema kuwa wanajisikia fahari kupiga hatua kimafanikio
tofauti na mwaka 2022 kwa kutekeleza adhima ya kuwahudumia wateja wao kalingana
na wanajipanga na kujiwekea mikakati imara katika kufanikisha malengo.
Anaweka wazi kuwa hali hiyo ya kupiga hatua inawapa moyo na
kuwaongezea ufanishi katika mikakati yao mbalimbali ya shughuli za kijamii
inayofanikisha kujiendesha kwa faida.
“Benki ilipata faida kabla ya kodi y ash. Mil 1,984 kwa mwaka
ulioishia desemba 31 mwaka 2022 (2021: TZS milioni 706 ) na mapato baada ya
kodi yalikuwa sh. mil. 1,416 ikiwa ni ukuaji wa 141% ikilinganishwa na sh. mil.
Tsh 587 mwa”ka 2021.
“Katika mwaka huo juhudi kubwa zilifanywa ambapo
faida ya benki iliongezeka kwa sababu ya kutafuta njia mpya za biashara na
kuendelea kutoa huduma za kiushindani,” amesema.
Tarimo, amefafanua kuwa juhudi za uwekezaji
zilizofanywa katika mwaka huo zilisababisha ongezeko la 31% katika viwango vya
riba. Mapato halisi ya riba yalikua mwaka hadi mwaka hadi kufikia sh. mil. 9,911
kutoka sh. mil. 7,538 mwaka 2021.
Amesema ongezeko la mapato ya riba halisi ni
matokeo ya ongezeko la mikopo la sh. mil. 2, 942 kutoka baki ya mikopo ya sh.
57,716 mwaka 2021 hadi Tsh. mil. 60, 658 mwaka 2022 na riba ya uwekezaji katika dhamana
iliongezeka kwa sh. 1,667 kutoka sh. 2,089 mwaka 2021 hadi sh. mil. 3,756 mwaka
2022.
Baada ya mafanikio, Tarimo amesema malengo yao ya kimkakati ni kuwa benki ya kitaifa itakayokuwa na matawi katika mikoa mbalimbali ya Tanzania na wanaamini kwamba watafikia adhima hiyo katika kipindi cha miaka mitano ya mpango mkakati cha mwaka 2022 hadi 2026.
Naye Meneja wa Usajili Hisa na Hati Fungani, Gideon Kapange ametoa wito kwa wanahisa wote ili wafanikishe mchakato wa kuchukua fedha wanatakiwa kupeleka taarifa zao mapema na ili kupata taarifa kamili wanapatikana kwa simu 0746140516.
“Hadi
sasa wapo baadhi ya wanahisa ambao hatuna taarifa zao kutokana na sababu
mbalimbali ikiwamo wakati walipokuwa wakijisalijili hawakuwa wamekamilisha
taarifa zao.




No comments:
Post a Comment