KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UWEKEZAJI WA MITAJI YA UMMA (PIC) YARIDHISHWA NA UJENZI WA SGR, YAIPONGEZA TRC - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Wednesday, March 27, 2024

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UWEKEZAJI WA MITAJI YA UMMA (PIC) YARIDHISHWA NA UJENZI WA SGR, YAIPONGEZA TRC

Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye ni Mbunge wa Kasulu Vijijni, Augustine Vuma, amezungumza hayo leo Machi 27, 2024 mkoani Morogoro kabla ya kurejea Dar es Salaam wakati akitoa majumuisho ya ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa reli hiyo na kuangalia majaribio ya usafiri huo unaotarajiwa kuanza safari zake Julai mwaka huu.


NA MAGENDELA HAMISI

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji ya Mitaji ya Umma (PIC), imeridhishwa pasipo na shaka na mradi wa ujenzi wa reli ya umeme (SGR) kutoka Dar es Salaam, Morogoro hadi Dodoma na kutoa rai kwa Shirika la Reli Tanzania (TRC), kutunza miundo mbinu ya reli na kuwasimamia vema  wakandarasi ili wamalize kazi kwa wakati.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye ni Mbunge wa Kasulu Vijijni, Augustine Vuma, amezungumza hayo leo Machi 27, 2024 mkoani Morogoro kabla ya kurejea Dar es Salaam wakati akitoa majumuisho ya ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa reli hiyo na kuangalia majaribio ya usafiri huo unaotarajiwa kuanza safari zake Julai mwaka huu.

“Kamati tumeridhishwa pasipo na shaka kwamba mradi huu umetenenezwa kwa kiwango cha stahiki na unavutia kwa watanzania na tumeelezwa pindi ukikamilika utakuwa na faida nyingi kwa maana tayati umetoa ajira za moja kwa moja 30,000 na zisizo za moja kwa moja 150, 000 ambazo zimewezesha kipato cha shilingi bilioni 350.

“Pia tumeambiwa safari zitakapoanza zitapunguza nusu ya muda wa kusafiri unaotumika na mabasi kutoka Dar es Salaam, Morogoro hadi Dodoma na tunaamini Watanzania watatumia muda mfupi katika safari na kusafirisha mizigo na tunaona kabisha inakwenda kufanikiwa,” amesema.

Ameongeza kuwa kutokana na hatua ambayo imefikiwa ya ujenzi na majaribio ya safari kwa niaba ya kamati hiyo anaipongeza Serikali chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa ambayo imefanyika na kutoa fedha kwa ajili ya mradi huo ambao unaonekana unakwenda kuwa na faida kubwa kwa taifa na wananchi kwa ujumla.

Pia aliipongeza TRC kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa mradi huo ambao upo katika hatua za mwisho kukamilika kwa njia ya Dar es Salaam Morogoro hadi Dodoma na dhahiri Julai safari zitaanza kama ambavyo Rais Dkt Samia ameagiza.

Ameongeza kuwa hadi kukamilika kwa mradi huo, Serikali itakuwa imetumia Dola million 10 sawa na sh. trillion 23 za kitanzania na tayari imetumia asilimia 40 ya fedha hizo na kutoa rai kwa watanzania kutumia fursa ya uwepo wa reli hiyo kibiashara itakayowaongezea kipato kwa kusafirisha mizigo kwa bei nafuu.

Naye Mwenyekiti wa Bodi TRC, Ally Kalavina kutokana na mradi huo ulipofikia na watakiwa katika majaribio ya safari kutoka Dar hadi Morogoro ni dhahiri watatekeleza maagizo ya Rais Dkt Samia kwa wakati ifikapo Julai kwa safari kuanza rasmi ya kubeba abiria na mizigo, Dar es Salaam kwenda Dodoma.

“Vitu vingi vimekamilika yaliyobaki ni maeneo madogo ambayo yanaendelea kufanyiwa kazi ili kuhakikisha yanakamilika kwa wakati uliopangwa na niwaondoe hofu Watanzania kuwa wawe na amani kwani tren zitaanza kufanya kazi kwa wakati,” amesema.

Pia Mkurugenzi wa TRC, Masanja  Kadogosa amesema wanaishukuru kamati hiyo kwa kukagua ujenzi na huo na majaribio na kuridhishwa na hatua ambayo imefikiwa kwa sasa na kusisitiza kuwa mchakato wa nauli upo chini Mamlaka ya Udhibiti Usafari wa Ardhini (LATRA) na kabla ya Julai zitatangazwa kwa wananchi.

“Kwa upande wetu tumeshakamilisha michakato inayotuhuu na hatua iliyobaki ni kwa Latra ambayo tayari wameshafanya majadilino na baadhi ya wadau na pindi watakapokalisha watatangaza nauli kabla ya Julai,” amesema.Mkurugenzi wa  Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja  Kadogosa (kulia) akiwa na Mwenyekiti wa Bodi TRC, Ally Kalavina kwenye treni ya umeme (SGR) wakienda Morogoro kutokea Dar es Salaam.



No comments:

Post a Comment