MAADHIMISHO YA MIAKA 60 YA JWTZ KUANZA JULAI 25 - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Wednesday, July 3, 2024

MAADHIMISHO YA MIAKA 60 YA JWTZ KUANZA JULAI 25


NA MAGENDELA HAMISI

JESHI la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) limetangaza rasmi kukamilika kwa maandalizi ya maadhimisho ya miaka 60 tangu kuasisiwa kwake Septemba Mosi 1964, chini ya Hayati Mwalimu Julius Nyerere, yatakayoanza rasmi Julai 25,2024 na kuhitimishwa Agosti 23, mwaka huu.

Akitoa taarifa hiyo leo, Julai 3, 2024 mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam,  Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa JWTZ, Luteni Kanali Gaudentius Ilonda, maadhimisho yashirikisha Kamandi zote za kijeshi ambazo zitafanya mazoezi katika nchi kavu na baharini.

“Nawaomba wananchi kwa kipindi chote cha maadhimisho hayo makubwa wasiwe na taharuki kwa kuwa ni ya kawaida ingawa yatakuwa ya kihistoria tangu kuasisiwa kwa JWTZ na yatabaki vichwani mwa vizazi hadi kizazi,” amesema.

Luteni Kanali, Ilondo ambaye pia ni Msemaji wa Jeshi hilo amefafanua kuwa za kijeshi zitakazokuwemo ni Jeshi la Anga, Jeshi la Wanamaji, Jeshi la Nchi Kavu, Jeshi la Akiba, Jeshi la Akiba na Vikosi Maalumu

 Pia ameweka wazi kuwa majeshi hayo yatafanya mazoezi hayo ya maadhimisho katika katika mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Pwani, Morogoro, Mbeya na Zanzibar sanjari hilo watakuwa wakitoa huduma za kijamii kwa wananchi kupata vipimo na matibabu bure.

Katika nyanja ya matibabu, tutaweza kupima magonjwa yanayoambukiza na yasiyoambukiza mfano, tutapima tezi dume kwa njia ya damu, kisukari, presha, VVU, Shinikizo la juu na chini la damu, pia tutahamasiha na kuchangia damu ili kuzipeleka kwa wahitaji maalumu ikiwemo kwa akina mama wanaojifungua na kusaidia wananchi wanaopata ajali na vituo vitakavyotumika ni vya Hospitali za Jeshi za Kanda ikiwamo Arusha, Mwanza, Mbeya Tabora na Zanzibar na kwa Dar es Salaam Meli kubwa itatia nanga na kutoa huduma za kimatiibabu kwa wananchi na itakuwa ni kama sehemu ya utalii na meli hiyo itawasili Julai 16, mwaka huu na tunawomba wananchi wajitokeze kwa wingi” amesema.

Ameongeza kuwa kutakuwa na vituo vingine vya kutolea huduma ya matibabu katika maeneo mbalimbali nchini na kwa Dar es Salaam, kituo kitakuwa Mbagala, Pwani kitakuwa eneo la Mapinga, Ruvuma katika eneo la Luhiko, Pemba na Unguja.

Luteni Kanali Ilondo ameingeza kuwa maadhimisho hayo pia yatahusisha gwaride kubwa litakolokuwa na sura ya miaka 60 na kutakuwa na zoezi la pamoja kati ya Serikali ya Tanzania kupitia JWTZ na Serikali ya Watu wa China kupitia, Jeshi la Ukombozi la Watu wa China.

Amefafanua kuwa zoezi hilo la pamoja kwa majeshi hayo yatafanyika Julai 29, 2024 na kuhitimishwa 11, Agosti mwaka huu na Tanzania ndio watakuwa wenyeji na litafanyika nchi kavu na baharini  na lengo ni kuhadhimisha miaka 60 ya ushirikiano wa pamoja kati waasisi wa mataifa ya Tanzania na China.

 “Maadhimisho hayo yanafanyika chini ya Mkuu wa Majeshi nchini na yatasimamiwa na Kamandi ya Nchi Kavu na wananchi wataweza kuona zana mbalimbali za kivita zinazotumiwa na majeshi yetu katika kujilinda na kuiweka nchi salama,” amesema.

Ameongeza kuwa katika maandimisho hayo pia kutakuwa na Mashindano ya Mkuu wa Majeshi ya Utamaduni ambayo yametokana na maono yake ambayo yanafanyika kwa mara ya kwanza nchini.

Tofauti na uwepo wa mashindano ya utamaduni pia kutakuwepo kwa mashindano ya CDF ambayo yatatolewa maelezo zaidi na kamati husika wakati wowote na wananchi watajulishwa.

No comments:

Post a Comment