MTUMISHI WA SUMA JKT-TUNDUMA AKWEPA KIFUNGO CHA MIAKA MITATU JELA ALIPA FAINI - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Wednesday, August 21, 2024

MTUMISHI WA SUMA JKT-TUNDUMA AKWEPA KIFUNGO CHA MIAKA MITATU JELA ALIPA FAINI


NA MWANDISHI WETU, SONGWE

MAHAKAMA ya Wilaya ya Momba Imemhukumu Esau Andrew Hinjo, aliyekuwa Askari wa SUMA JKT-TUNDUMA  adhabu ya kwenda Jela  miaka mitatu au kulipa faini ya sh. 500,000/- kwa kosa la kuomba na kupokea Hongo Kinyume na Kifungu cha 15(1) (a) na 2 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura 329 Marejeo ya Mwaka 2022.


Hukumu dhidi ya Esau Andrew Hinjo imetolewa  katika Kesi ya Rushwa Na.23763/2024 Agosti 21, 2024 mbele ya Hakimu Mkazi Mh. Claud Msenjelwa wa Mahakama ya Wilaya ya Momba.


Kesi hiyo imeendeshwa na Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU , Lilian Matara.


Ilielezwa kuwa Mshtakiwa alifikishwa Mahakamani kwa shtaka la Kupokea Hongo Kiasi cha sh.120,000/- toka kwa  Joseph Itera Chunche kama kishawishi cha yeye kutokamata nyavu haramu za kuvulia Samaki.


Mshtakiwa alikiri makosa yake na kulipa faini ya sh.500,000/-

No comments:

Post a Comment