MAFUFU, SHAMSA WAJIUNGA CCM, KUFANYA ZIARA KUELEZA MAFANIKIO YA DKT SAMIA - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Thursday, February 20, 2025

MAFUFU, SHAMSA WAJIUNGA CCM, KUFANYA ZIARA KUELEZA MAFANIKIO YA DKT SAMIA



NA MWANDISHI WETU

MASTAA wa filamu, Jimmy Mafufu na Shamsa Ford wamejiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) na sasa wakiwa chini ya Taasisi ya Mabalozi wa Mama wanaanza ziara nchi nzima kutangaza mafanikio ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan wakiwa na kaulimbiu ‘Asante Mama’.

Nyota hao wa filamu nchini wameamua kujiunga CCM wakitokea Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wanakiri sababu kubwa ya kuchukua uamuzi huo ni kutokana na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo iliyofanywa na Dkt Samia ambayo inafanya taifa kukua kiuchumi.

Mafufu akizungumza leo jijini Dar es Salaam amesema "tumeamua kujiunga CCM baada ya kubaini kupitia Serikali ya Awamu ya Sita imefanya makubwa kwa Watanzania tukiwemo wasanii ambao tumepewa mikopo ambayo imetusaidia kuinua kazi zetu.

“Licha ya kwamba mimi na Shamsha tulikuwa upinzani, mikopo hiyo inayotolewa na Rais wetu kwa wasanii haikutubagua, pia Serikali yetu imefanya mambo makubwa ikiwemo utekelezaji wa miradi ya kimaendeleo kama Barabara, Bwawa la Mwalimu Nyerere, Reli ya SGR, ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Msalato, hayo ni sehemu yaliyotukusukuma kujiunga CCM,” amesema.

Amesisitiza kwamba tangu Rais Dkt Samia, aingie madarakani ajashindwa, ametekeleza miradi yote iliyoachwa na marehemu Rais Dkt John Magufuli, hali ambayo imefanya kutoona umuhimu wa kubaki upinzani.

Wasanii hao wameungana na wasanii wengine akiwemo Salum Mchoma (Chiki), Single Mtambalike ‘Richt Ritch’, Rashidi Mwishehe ‘Kingwendu’ Abdallah Mkumbila ‘Muhogo Mchungu’.


Wengine ni wa muziki wa kizazi kipya akiwemo Boniventure Kabongo ‘Stamina, Juma Kassim ‘Nature ‘Sir Nature’, Amani Temba ‘Capt Temba, Richard Shauri ‘Ritch One’ na wengine na lengo lao ni kutangaza miradi yote ambayo imetekelezwa chini ya Rais Samia.

Shamsa naye amesema kwamba anajivunia kujiunga na CCM na kutoa wito kwa wasanii wengine ambao wako katika vyama vya upinzani kujiunga na ccm ili kuunganisha nguvu ya pamoja kutangaza miradi ya maendeleo ambayo imefanikisha kustawisha uchumi wa Tanzania.

Pia Ritch Ritch ambaye ni diwani wa CCM , amesema kuwa yeye ndiye kiongozi wa madiwani wote hivyo anaamini watatangaza, miradi yote ambayo imefanya vizuri kwa maslahi ya watanzania ili kila mmoja ajue namna Serikali ilivyofanikiwa  kupitia miradi ya Elimu, Usafiri wa Anga na mingineyo inayofanya Tanzania kuwa mfano wa kuigwa katika mataifa mengine.

No comments:

Post a Comment