PROFESA MKENDA AFUNGUA KONGAMANO LA 18 JIJINI DAR ES SALAAM - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Wednesday, May 7, 2025

PROFESA MKENDA AFUNGUA KONGAMANO LA 18 JIJINI DAR ES SALAAM


NA MWANDISHI WETU 

‎JUMLA ya mawaziri 20 kutoka   nchi mbalimbali duniani  wameudhuria  mkutano  18  unaofanyika kwa mara ya pili Tanzania unaohusu elimu mtandao (eLearning Africa).

‎ 

‎Mkutano  huo wa eLearning Africa ni heshima kwa nchi yetu  wenye lengo la kubadirishana mawazo na uzoefu   jinsi ya kutumia Digital  System kwa ajili ya utoaji masuala ya Elimu   ,

‎ Akizungumza katika mkutano  ndani leo Mei 7,2025  unaofanyika katika Ukumbi wa Mikutayo ya Kimataifa wa Julius Nyerere (JNCC )Jijini Dar es Salaam , Profesa Adolf Mkenda amesema Tanzania wanajitaidi sana kutumia Mfumo wa elearning pamoja na kwamba hawajasambaza vya kutosha  pia kuna njia za kutosha kwa kushirikiana na mashirika mbalimbali yasio ya Kiserikali ili shule mbalimbali ziweze kufikiwa .

‎"Nchi yetu leo imepata heshima ya mkutano mkubwa wa 18  wa eLearning Afrika  kufanyika na uliohudhuriwa na Mawaziri 20 kwa ajili ya kubadirisha mawazo pamoja na uzoefu" alisema Profesa Mkenda  

‎Profesa Mkenda alisema  watakikisha shule nyingi zinafikiwa na mfumo wa TEHAMA  kwa ajili ya kujifunza kompyuta na walimu wote wapewe vishikwambi  kwa ajili ya kusomea kwa sababu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan alitoa agizo walimu wote wapatiwe Vishikwambi..

‎Aidha, alisema elimu mtandao ni nyenzo muhimu  ya kufundishia pia sisi wenyewe tuwe na teknolojia ya akili mnemba   ambapo alisema Serikali imeruhusu shule  kuanzishwa Zanzibar na mfumo huo utachukua wanafunzi  watakaojifunza.

‎Pia alisema kozi kama hizo  zinatolewa katika chuo kikuu  cha Dodoma na Nelson Mandela Arusha lakini pia  bajeti ya mwaka huu wanafunzi wa kidato cha sita wanaofanya mitihani sasa hivi watakapata ufadhili wa masomo kama hayo.




No comments:

Post a Comment