CUF WAINYOOSHEA KIDOLE KURA YA MAPEMA ZANZIBAR - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Friday, August 8, 2025

CUF WAINYOOSHEA KIDOLE KURA YA MAPEMA ZANZIBAR



*KUFANYA MKUTANO MKUU MAALUMU KESHO


NA MWANDISHI WETU

 

MWENYEKITI Taifa wa Chama Cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba amesema ni aibu kuwepo kwa Kura ya Mapema kwa upande wa Zanzibar katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu Tanzania Bara na Zanzibar.

 

“Ni aibu kubwa kuwepo kwa kura ya mapema inayopigwa Oktoba 28 na Oktoba 29, 2025 wanachi wote wenye sifa ya kupiga kura ndio tunakuwa na jukumu hilo, sasa basi tunachaofanya sasa ni kuhakikisha katika uchaguzi huo tunapata wawakilishi wengi ili sheria hiyo ikabailishwe kwenye Baraza la Wawakilishi.

 

“Chama Cha Mapinduzi kilipata nafasi ya kupitisha sheria hiyo baada ya CUF kususia uchaguzi wa marudio mwaka 2016 na athari yake  ni kubwa, mwaka huu hatususii uchaguzi tunaingia kingangali ili tuweze kupata Wawakilishi wa kutosha ili sheria wakaipiginie ibarishwe,” amesema Prof Lipumba.

 

 

Prof Lipumba amebainisha hayo leo Agosti 8, 2025 jijini Dar es Salaam wakati akitoa taarifa ya kufanyika Mkutano Mkuu Maalumu wa kupitisha wagombea wa Urais.upande wa Tanzania pna Tanzania Zanzibar waliopendekezwa na Baraza Kuu la Uongozi Taifa la Chama hicho Agosti 6 mwaka huu.

 

Ameongeza kwamba wagombea waliopendekezwa kwa upande wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Gombo Sambandito Gombo na Nkunyuntila Siwale kwa upande wa Zanzibar waliopendekezwa kugombea nafasi hiyo ni watatu ambao ni Mhandisi Mohamed Habib Mnyaa, Mhandisi Hamad Masoud Hamad na Dkt..Mohamed Habib Mikidadi.

 

Wagombea hao watapigiwa kura na wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalum ili kupata mgombea mmoja atakayepeperusha bendera ya CUF katika kampeni za Uchaguzi Mkuu Oktoba Mwaka huu.

 

Wakati huo huo, Prof. Lipumba amesema katika mkutano huo, watazindua Ilani yao kwa ajili ya kutangaza sera za chama kwa wananchi kwenye kampeni za uchaguzi mkuu ili wananchi waweze kuendelea kukiamini na kukipa ridhaa ya kushika dola. 

 

"Baraza kuu la Uongozi Taifa limepokea na kupitisha rasimu ya Ilani ya Uchaguzi Mkuu upande wa Muungano,pamoja na rasimu ya Uchaguzi Mkuu upande wa Zanzibar na Kupitisha wagombea wa ubunge,vilevile wagombea wa uwakilishi"amesema Prof. Lipumba. 

 

Aidha amesema kuwa Ilani ya CUF imebeba maono ya kujenga Tanzania Mpya kupitia Serikali ya umoja wa kitaifa yenye misingi imara,ya usawa,  mshikamano, uwajibikaji, demokrasia ya kweli na maendeleo jumuishi kwa watu wote.

 

"Ilani ya CUF imejikita katika misingi yakuweza kuleta haki sawa na furaha kwa Wananchi wote,kujenga uchumi jumuishi unao ongeza ajira na kuondoa umasikini,kuimarisha misingi ya demokrasia na utawala wa Sheria kwa kupata katiba mpya inayotokana na maoni ya Wananchi,kuweka msingi wa maendeleo endelevu kwa kufanikisha utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu(Sustainable Development Goals) ifikapo mwaka 2030.

 

“Pia Ilani yetu inatekeleza Sera ya CUF ya kipato cha msingi ni haki ya kila Mtanzania kwa kuanza kuwalipa wazee wote wenye miaka kuanzia 60 nakuendelea kipato cha kujikimu na tunaamini uchaguzi huu ukiwa huru nawa haki wagombea wetu watapata Ushindi mnene kwenye uchaguzi huo,” amesema.

 


No comments:

Post a Comment