MAZISHI YA GABRIEL MWAIBALE: MCHUNGAJI KLPT AHIMIZA MAISHA YA KUMJUA MUNGU - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Sunday, July 19, 2026

MAZISHI YA GABRIEL MWAIBALE: MCHUNGAJI KLPT AHIMIZA MAISHA YA KUMJUA MUNGU

Waombolezaji wakishusha kaburini jeneza lenye mwili wa Gabriel Ambakisye Mwaibale wakati wa mazishi yake yaliyofanyika Makaburi ya City Yombo Dovya Temeke Jijini Dar es Salaam Julai 16, 2026.

............................................

Wanadamu tumetakiwa kuishi maisha ya kumjua Mungu kwani hapa duniani ni wageni tunapita.

Ombi hilo limetolewa na Mchungaji Michael Ndimbwa wa Kanisa la Pentekoste Tanzania (KLPT) Tandika Jijini Dar es Salaam wakati akiongoza ibada ya mazishi ya Gabriel Mwaibale iliyofanyika Julai 16, 2026 Yombo Dovya Njia Panda ya kwa Mwinyi.

Alisema msiba wowote unaleta huzuni kwa kuondokewa na mpendwa wao.

“Maisha ya aliyefariki yana maana kwa wale wanaoguswa naye na kama hayana mguso yanakuwa hayana maana,’ alisema Ndimbwa.

Alisema hapa duniani sisi wote ni wageni hivyo tunapaswa kujua maisha yetu si kitu chochote mbele ya Mwenyezi Mungu.

Ndimbwa alisema kila mtu anapaswa kuishi maisha yenye maana ya kumjua Mungu badala ya kutegemea mambo ya duniani.

Akitolea mfano wa tajiri mmoja ambaye alilazimika kuuza mali na gari lake la kifahari baada ya kupata ugonjwa wa moyo ili atafute maisha yenye maana.

Alisema changamoto kubwa tuliyonayo ni kushindwa kujitambua kwani mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake siyo nyingi hivyo kila mmoja wetu anapaswa kujiuliza kama anaishi maisha ya maana.

Alisema maisha ya kumjua Mungu yana changamoto kubwa mbele ya dunia lakini mbele ya Mungu yatamfanya mtu anaye muamini kuwa salama.

“Kila mtu atafakari safari ya maisha yake hapa duniani na uamuzi wa kufanya kati ya kutafuta maisha yasiyo na maana au yenye maana,” alisema Mchnguaji Ndimbwa.

Diwani wa Kata ya Makangarawe wilayani Temeke, Fadhil Mboga, akitoa salamu za rambirambi wakati wa ibada hiyo aliwashukuru viongozi mbalimbali, wakiwepo wa dini zaidi ya 10 na wananchi walioshiriki kwenye msiba huo na kusisitiza ushirikiano huo uzidi kuendelea.

Mazishi ya Gabriel Ambakisye Mwaibale ambaye alifariki Julai 14, 2026 Hosptali ya Rufaa ya Temeke alikokuwa akitibiwa kutokana na maradhi ya figo yalifanyika Julai 16, 2026 katika Makaburi ya City Yombo Dovya.

Mchungaji Michael Ndimbwa wa Kanisa la Pentekoste Tanzania (KLPT) Tandika Jijini Dar es Salaam, akiongoza ibada ya mazishi ya Gabriel Mwaibale.
Baba wa Gabriel Mwaibale akiwa ameshika tama wakati wa ibada hiyo.
Mama Mzazi wa Gabriel Mwaibale akilia kwa uchungu.
Jirani wa Wazazi wa marehemu,  Mzee Alexander Mwakalasya akiwajibika ipasavyo wakati wa msiba huo.
Mchungaji Justine Kiwovewe (kushoto) na Mchungaji Michael Ndimbwa wa Kanisa la
KLPT wakiombea jeneza lenye mwili wa Gabriel wakati wa ibada hiyo.
Marehemu Gabriel Mwaibale enzi za uhai wake.
Waombolezaji, ndugu, jamaa, marafiki na majirani wakiwa kwenye ibada hiyo.Diwani wa Kata ya Makangarawe,  Fadhil Mboga akitoa salamu za rambi rambiIbada ya mazishi ikiendelea.Ibada ya mazishi ikiendelea.Kwaya ya Kanisa la KLPT ikiimba nyimbo za maombolezo wakati wa ibada hiyo.Viongozi wa dini wakiwa kwenye ibada hiyo.Waombolezaji wakiwa kwenye ibada hiyo. Kushoto ni jirani wa wazazi wa marehemu, Christopher Mwamasaga.Huzuni ukitamalaki kwenye msiba huo.Heshima za mwisho zikitolewa.Dada wa marehemu Ambwene Kyoga akitoa heshima za mwisho.Heshima za mwisho zikitolewa.Jirani ya wazazi wa marehemu Christopher Mwamasaga akitoa heshima za mwisho.Dada wa marehemu Mary Anyitike akitoa heshima za mwisho.Kaka wa marehemu Dotto Mwaibale akitoa heshima za mwisho.Ni vilio na huzuni wakati wa msiba huo.Dada wa marehemu Naomi na Elnes wakilia kwa uchungu wakati wakiaga mwili wa mdogo wao Gabriel.Dada wa Marehemu Gabriel, Elnes Mwamasangula akilia kwa uchungu wakati wa ibada ya kumuaga mdogo wake.Heshima za mwisho zikiendelea kutolewa.Mama wa marehemu Gabriel akimuaga mwanaye.Jeneza lenye mwili wa Gabriel likiwa limebebwa na waombolezaji.
Mchungaji Yohana Maimba wa Kanisa la KLPT Keko akiongoza mazishi ya Gabriel.
Baba wa marehemu akiweka shada kwenye kaburi na mtoto wake.Waombolezaji wakiwa kwenye msiba huo.Baba wa marehemu akifarijiwa.Huzuni na majonzi ukitawala kwenye msiba huo.Ni huzuni katika msiba huo.Viongozi wa dini kutoka makanisa mbalimbali wakiwa kwenye ibada ya kumuaga marehemu. Waombolezaji wakitupa udongo kaburini wakati wa mazishi ya mpendwa wao. Kushoto mwenye chepe lenye udongo ni Kaka wa marehemu Amon Papobali.

Kaka wa marehemu, Aswile Mwaibale akiwa amebeba msalaba wakati wa mazishi.
Kaka wa marehemu Kulwa Mwaibale akimfariji mama mkubwa wa Gabriel wakati wa uagaji wa mwili.Ndugu wa marehemu Gabriel, Andrew Nunkongile (katikati), ambaye alisimamia itifaki ya kuaga mwili akiwajibika.
Jirani wa Wazazi wa marehemu Anthony Mwakanyamale akitoa heshima za mwisho.
Wana ndugu wa marehemu wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazishi.

Habari hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale simu namba 0754362990.

No comments:

Post a Comment