NA SIXMUND BEGASHE
KAMATI ya Maandalizi ya maadhimisho ya wiki ya Mradi wa Kuboresha Usimamizi wa Maliasili na Kukuza Utalii Kusini mwa Tanzania (REGROW), imekutana kwa kikao chake cha pili Mkoani Iringa ili kupata uwelewa wa pamoja na kuweka mikakati ya utekelezaji na ufanikishaji wa maadhimisho hayo.
Naye Naibu Msimamizi wa Mradi wa REGROW Wizara ya Maliasili na Utalii Bi. Blanka Tengia, amefafanua kuwa mradi huo unaboresha miundombinu na kuzijengea uwezo wa kusimamia hifadhi za kipaumbele kwa lengo la kuziwezesha kutunza maliasili.
Kamati hiyo inajumuisha wajumbe kutoka TANAPA, Maafisa mbalimbali wa Serikali ya Mkoa wa Iringa, Jeshi la Polisi na Maafisa watekelezaji wa mradi wa REGROW Wizara ya Maliasili na Utalii, Bodi ya Utalii na Wakala wa Huduma za Misitu.







No comments:
Post a Comment