MSAJILI AKUTANA NA VIONGOZI WA CHADEMA KUJADILI KUIMARISHA DEMOKRASIA NCHINI - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Thursday, August 24, 2023

MSAJILI AKUTANA NA VIONGOZI WA CHADEMA KUJADILI KUIMARISHA DEMOKRASIA NCHINI


1.    Mwenyekitiwa CHADEMA, Freeman Aikael Mbowe (kushoto), akisisitiza jambo mbele ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, wakati wa kikao cha Msajili na viongozi waandamizi wa CHADEMA leo jijini Dar es Salaam. Kikao cha Msajili na CHADEMA ni juhudi za ofisi hiyo kuimarisha hali ya kisiasa hususan demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini. 

1.    Mwenyekitiwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mheshimiwa Freeman Aikael Mbowe (kulia) akiteta jambo na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi (katikati), baada ya kumaliza kikao chenye lengo la kuimarisha demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini kilichofanyika kwenye ofisi ndogo za Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa mtaa wa Shaaban Robert jijini Dar es Salaam. Pembeni ni Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Myika.

NA MWANDISHI WETU

MSAJILI wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, leo jijini Dar es Salaam amekutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa CHADEMA mheshimiwa Freeman Aikael Mbowe yenye lengo la kuimarisha mazingira ya siasa hususani demokrasia ya vyama vingi vya siasa. 

Viongozi wa CHADEMA walioambatana na Mbowe kwenye kikao hicho na Jaji Mutungi ni pamoja na Katibu Mkuu wa CHADEMA , John Mnyinka na Katibu wa Baraza la Wazee (BAZECHA),  Rodrick Rutembeka.

No comments:

Post a Comment