*GST YAENDELEA KUITANGAZA KITABU KINACHOONESHA MADINI YANAYOPATIKANA TANZANIA
MAONESHA ya Kwanza ya Madini yanayoendelea wilayani Ruangwa Mkoa wa Lindi katika viwanja Kilimani Hewa yaliyobebwa na Kaulimbiu ya isemayo "Wekeza Lindi kwa Ukuaji wa Uchumi na Maendeleo ya Jamii yaendelea kutembelewa na wadau mbalimbali wa Sekta ya Madini.
Katika Maonesho hayo, Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) inaendelea kutoa elimu ya taarifa za tafiti za Madini mbalimbali yapatikanayo nchini Tanzania kilichotolewa Mwaka 2023.
Kwa upande wake, Meneja wa Sehemu ya Jiolojia Maswi Solomon amesema GST imejipanga
kusambaza vitabu vinavyoanesha Madini yapatikanayo Tanzania kwa Wakuu Mikoa na
Wilaya kote nchini zoezi linaloenda sambamba na uelimishaji wa masuala
mbalimbali ya jiolojia na madini katika mikoa husika.
Pamoja na mambo mengine, Maswi ametoa wito kwa wadau mbalimbali wa Sekta ya Madini kufika katika Banda hilo ajili ya kujipatia nakala ya Kitabu cha Madini pamoja na kujipatia elimu na muongozo wa tafiti zilizofanyika nchini ikiwemo uchunguzi na utambuzi wa sampuli za Madini, Uchenjuaji, na elimu ya tabia za miamba.
Pia, Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) kinaendelea
kutangaza bidhaa na huduma zake ikiwemo vidani, Pete, vikuku, mikufu, hereni
pamoja na nafasi za mafunzo ya uengezaji thamani wa madini ya vito ambapo wadau
mbalimbali wanaendelea kutembelea banda hilo kwa ajili ya kuchukua fomu za
kujiunga na chuo hicho.
No comments:
Post a Comment