Akizungumza katika ziara ya kamati hiyo Mwenyekiti wa Kamati, Daniel Sillo, amesema kukamilika kwa mradi huo ,kutaongeza pato la mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla, hivyo mradi huo pamoja na miradi mingine, itachangia ongezeko la fedha katika bajeti ya Serikali.
Aidha, Naibu Waziri wa Kilimo, David Silinde, amempongeza Mkurugenzi Mkuu Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Raymond Mndolwa ,kwa usimamizi thabiti wa miradi ya ujenzi, miundombinu ya umwagiliaji.
Sanjari na hayo, Silinde amewaasa wakulima wa eneo hilo kuutunza na kuulinda mradi huo, ili uwe na tija, katika kukuza sekta ya umwagiliaji nchini.
Hata hivyo, Mkurugenzi Mkuu Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Mndolwa amesema, Tume itahakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati kama ilivyopangwa, ambapo hadi sasa mradi umefikia 95%,ambapo jumla wakulima 2400 watanufaika.
Mndolwa ameongeza kuwa, miradi yote inayojengwa itakamilika kwa wakati, na Serikali inaendelea kutoa fedha kwa aajili ya utekelezaji.
Mradi wa ujenzi bwawa la umwagiliaji Tlawi, baada ya kukamilika,utaongeza eneo la umwagiliaji kutoka Hekta 5 mpaka zaidi ya Hekta 90,na wakulima wataweza kulima msimu mmoja hadi mitatu kwa mwaka,pamoja na kuzalisha ajira kwa jamii inayozunguka mradi huo.











No comments:
Post a Comment