Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Dkt. Anna Henga akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Aprili 4, 2024
NA MWANDISHI WETU
KITUO cha Sheria na
Haki za Binadamu (LHRC) kimetoa wito kwa Serikali kuwasilisha Muswada wa Sheria
utakaotoa fursa ya kufanya mabadiliko ya Katiba ili kuruhusu baadhi ya masuala
ambayo kwa uasili wake hayawezi kufanyiwa marekebisho bila kugusa Katiba.
Hayo yamebainishwa leo
April 4, jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Dkt. Anna Henga wakati
akizungumza na waandishi wa habari na kuchambua sheria uchaguzi baada ya
kusainiwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na kupongeza baadhi ya maoni yao
ambayo yamefanyiwa kazi.
Amesema kuwa wameamua
kutoa tamko hilo kwa kuwa LHRC wamehusika kwa njia moja au nyingine kuwasilisha
maoni yao mbele ya Kamati ya Bunge ya Uwatawala, Katiba na Sheria jijini Dodoma
ili kuboresha mfumo wa Uchaguzi na Vyama Vya Siasa.
“Wakati inaletwa
miswada hiyo hakika kulikuwa na matumaini mapya kwa taifa letu kutokana na kiu
ya muda mrefu kuhusu maboresho ya mfumo wa Uchaguzi na Vyama vya Siasa hapa
nchini ingawa tunarejea kutoa rai kwa Serikali kuleta mswada wa mabadiliko ya
Katiba, 2024 kwa lengo la kufanya maboresho yanayopendekezwa na wadau na ripoti
ya kikosi kazi cha Demokrasia ya vyama vingi iliyowasilishwa na Mwenyekiti wake
Prof. Rwekaza Mukandala Oktoba 21, 2022, amesema.
Amesema kuwa wamebaini
kuwa masuala chanya yaliyomo katika sheria mpya kuna changamoto ya Wakurugenzi
wa Halmashauri za Manisapaa, Jiji na Wilaya licha ya kuondolewa kuwa wasimamizi
wa Uchaguzi bado wamebaki kuwa waandikishaji wa uchaguzi.
Ameongeza kuwa sheria
imeweka sifa ya mtu kuwa Msimamizi wa Uchaguzi, Mosi, awe hajawahi kutiwa
hatiani katika shauri la nidhamu au kosa lolote la jinai, pili, awe hajawahi
kuadhibiwa kwa kifungo kinachozidi miezi sita na tatu, awe hajawahi kuwa
kiongozi wa chama cha siasa.
Pia amesema sheria
imefuta suala la wagombea kupita bila kupingwa katika ngazi zote (Rais, Ubunge
na Madiwani) na sharti la Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume
kufanyiwa usaili na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji
kusimamiwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.
Pia kufutwa kwa sharti
la kulipa ada yakupata upya kadi ya mpiga kura iliyoharibika au kupotea, pamoja
na mashauru ya Uchaguzi kusikilizwa ndani ya miezi sita, na nafasi ya kiti cha
Ubunge tofauti na pendekezo la miezi 12 kama ilivyokuwa kwenye Muswada.
"Hata hivyo
mashauru ya Uchaguzi kwa ngazi ya udiwani yatasikilizwa kwa miezi 12 ambayo
bado tunaona ni muda mrefu," amesema Dkt. Henga.





No comments:
Post a Comment