JAJI MKUU AITAKA BRELA KUIUNGANISHA MAHAKAMA KWENYE KANZIDATA - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Saturday, July 6, 2024

JAJI MKUU AITAKA BRELA KUIUNGANISHA MAHAKAMA KWENYE KANZIDATA


NA MWANDISHI WETU

 JAJI Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma ameitaka Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) kuiwezesha Mahakama nchini kuunganishwa kwenye Kanzidata ya Wakala ili kuweza kuhakiki taarifa za kampuni kwa uharaka pindi inapokuwa  inashughulikia mashauri yahusuyo kampuni hizo


Rai hiyo ameitoa leo tarehe 5 Juni, 2024 alipotembelea banda la BRELA lilipo ndani ya jengo la Wizara ya Viwanda na Biashara katika maonesho ya 48  ya kimataifa ya biashara ya Dar es Salaam.


Mhe. Prof. Ibrahim Juma amesema kuwa uunganishwaji katika kanzi data itaiwezesha Mahakama kujua uhai wa kampuni na endapo imehuisha taaifa zake kwa Msajili  hii itasaidia kuamua kuendelea na kesi au kusitisha endapo kampuni haijahuisha taarifa zake kwa Msajili


Aidha, Jaji Mkuu ameipongeza BRELA kwa kazi kubwa inayofanya katika kuboresha utoaji wa huduma zake kwa njia ya mtandao 


BRELA inashiriki katika kutoa huduma za papo kwa hapo kwenye maonesho ya 48 ya kimataifa ya biashara ya Dar es Salaam ndani ya banda la Wizara ya Viwanda na Biashara na banda karibu na Wizara ya Fedha na Mipango

No comments:

Post a Comment