RAIS DK SAMIA KUHUTUBIA MKUTANO WA FOCAC NCHINI CHINA - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Saturday, August 31, 2024

RAIS DK SAMIA KUHUTUBIA MKUTANO WA FOCAC NCHINI CHINA


NA HAMISI MRISHO

RAIS wa Jamhuri wa Muungano Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan,anatarajiwa kuhutubia katika Mkutano wa Tisa wa Kilele wa Wakuu Nchi na Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) utakaoanza Septemba 4 hadi 6 mwaka huu katika Jiji la Beijing nchini China.

Hayo yamebainishwa leo Agosti 31, 2024 jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mambo ya Ndani na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mahamoud Thabit Kombo wakati akizungumza na waandishi wa Habari kwa mara ya kwanza tangu kuteuliwa kushika nafasi hiyo na kubainisha kuwa Rais Samia katika mkutani huyo ataongoza ujumbe wa watu wa tano kutoka Tanzania.

“Rais Samia anashiriki mkutano huo baada ya kupata mwaliko kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Xi Jinping, na hayo ni mafanikio makubwa kwa Tanzania na unaendeleza ushirikiano ambao unatimiza miaka 60 tangu kuasisiwa kwake,” amesema.

.Ameongeza kuwa katika mkutano huo Tanzania na China zitawekeana saini ya kufanya maboresho ya reli ya Tazara ili kuifanya kuwa na ubora wa hali ya juu na kuanza kutumika mabehewa ya kisasa kutoka hapa Tanzania hadi Zambia jambo litakaloimarisha usafiri wa njia ya reli.

Amefafanua kuwa katika mkutani huyo Tanzania pia itajikita katika majadiliano katika nyanja mbili ya kilimo na uchumi wa viwanda ambayo itatoa fursa katika sekta ya uwekezaji ambayo ndio mahusus kwa sasa.

Ameongeza kuwa,utasaidia kuibua fursa mpya za ushirikiano kwa manufaa ya pande zote mbili pamoja na kutangaza maboresho makubwa yaliyofanywa na Serikali ya awamu ya Sita ya sera na sheria katika sekta ya biashara na uwekezaji ili kuvutia wawekezaji wengi zaidi kutoka nchini humo.

Amebaisha kuwa Kaulimbiu katika mkutano huo ni “Kushirikiana ili Kuendeleza Usasa na Kujenga Jamii Bora ya China na Afrika kwa Mustakabali wa Pamoja" na tayari mataifa 40 kati ya 54 ya Afrika yamethibitisha kushiriki hadi sasa.

Jukwaa la FOCAC lilianzishwa mwaka 2000 na Jamhuri ya Watu wa China kwa lengo la kukuza ushirikiano na maendeleo ya pamoja kati ya China na Afrika, ambapo tangu kuanzishwa kwake jumla ya mikutano ya Kilele (Wakuu wa Nchi na Serikali) nane imefanyika na inafanyika kila baada ya miaka mitatu.

Ameongeza kuwa mkutano huo wa tisa utafunguliwa na Rais wa China Jinping na atatoa hotuba yake ya ufunguzi itakayotoa uelekeo wa China katika uhusiano wake na nchi za Afrika, 

Mkutano huo utawakutanisha viongozi na wakuu wan chi za Afrika, wawakilishi wa mashirika ya kikanda ya Afrika, mashirika ya kimataifa na wadau wengine walioalikwa.

Baadhi ya viongozi walioalikwa na wanaotarajiwa kushiriki katika mkutano huo ni Antonia Guterres ambaye ni Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Moussa Faki ambaye ni Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika.

Balozi Kombo amefafanua kwamba katika mkutano huo mada zitakazojadiliwa ni nne ambazo ni Utawala wa Nchi, Mpango wa Miundombinu na Uwekezaji, Maendeleo ya Viwanda na Kilimo cha Kisasa na Amani na Usalama, kwa upande wa Tanzania utajikita kwenye mada ya Maendeleo ya Viwanda na Kilimo kutokana na kuzingatia Mpango wa Maendeleo wa Tatu wa Miaka Mitano, ambao ndiyo mpango wa mwisho wa utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Tanzania ya 2025.

Amesema Tanzania inatarajia kuwasilisha miradi mbalimbali ikiwemo mipya na ile ambayo haiweza kutelezwa kwenye mpango uliopita wa FOCAC kwa sababu mbalimbali, ili iweze kutekelezwa chini ya mpango kazi wa FOCAC kwa kipindi cha 2025-2027 kwa kupatiwa fedha za mkopo nafuu na msaada.

Miradi hiyo ni pamoja na Ujenzi wa Mtandao wa Mawasiliano Vijijini wa awamu ya pili, Ujenzi wa njia ya kusafirisha Umeme wa Kv 400 wa awamu ya Pili na Tatu , Ujenzi wa Vyuo vya Ufundi Stadi (VETA) wa awamu ya Pili na Ujenzi wa Babara za Zanzibar Zenye Urefu wa Kilomita 277.7 .

No comments:

Post a Comment