NA MWANDISHI WETU
CHAMA Cha Wananchi (CUF)
kimesema kuwa tayari ‘kimeshang’atwa na nyoka’ katika masuala ya kuunganisha vyama
vya siasa ili kusimamisha mgombea mmoja kwenye uchaguzi mkuu, hivyo hawataweza
kuingia katika mtegoni huo.
Akizungumza na Waandishi
jijini Dar es Salaam leo Machi 2, 2025 wakati akitoa msimamo wao kuelekea Uchaguzi Mkuu ujao, Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa
Ibrahim Lipumba amesema uchaguzi wa mwaka 2015 waliamini kuwa wanaunganisha
vyama kwa dhati, kumbe chama kingine kipo kimkakati kudhoofisha vingine kutokana
na uchu wa madaraka.
“Wakati ule tulipokuwa
UKAWA, nikiamini tuko pamoja wakati na narudisha fomu ya kugombea kiongozi
mmoja wa chama (jina kapuni) ambaye tulikuwa naye katika muungano huo alikuja
kuniwekea pingamizi dakika za mwisho jambo ambalo liliniumiza sana,” alisema.
Pia aliongeza kuwa
wakati wa ujazaji wa fomu kwa wagombea wa CUF, viongozi wa chama kingine (jina
kapuni) waliwashawishi wajaze kama wanatoka kwenye vyama vyao na hiyo
inadhihirisha walijipanga kudhoofisha vyama vingine.
Kulingana na changamoto
hizo zilizojitokeza wakati huo wa kuunganisha vyama kwa lengo la kuwa na nguvu
ya pamoja ili kuking’oa madarakani Chama Cha Mapinduzi (CCM), Prof Lipumba
amesema kwa sasa wako ngangali na hawaofii kuunganisha vyama kikubwa wataongeza
umakini.
Pia Prof Lipumba
amesisitiza kwamba wakati Uchaguzi Mkuu ujao ukiwa umebakisha miezi michache
kufanyika ni vizuri uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika mwaka jana
ukarudiwa akimiani haukuwa huru na haki.
Ameongeza kuwa tofauti
na uchaguzi huo kutaka urudiwe, pia amesisitiza Uchaguzi Mkuu ujao ufanyike
baada ya kufanyika marekebisho ya Sheria na Tume Huru ya Uchaguzi pamoja na
upatikanaji wa Katiba Mpya.
Wakati Prof Lipumba
akitoa misimamo hiyo, pia amewaka wazi kuwa kwa sasa kamati ya chama hicho
inayoshughulikia uwandaaji wa Ilani ya Uchaguzi inaendelea na mchakato huo kwa
kutumia akili Mnemba (AI) ili kupata mawazo mapana ya kusaidia kufikia malengo stahiki.
“Kamati yetu inaandaa
ilani ya uchaguzi kwa kutumia akili Mnemba na imani yetu itatatua changamoto
mbalimbali zilizopo na kupata ilani iliyobora, pia watanzania wanatakiwa
kufahamu kuwa uchaguzi ni gharama, hivyo watuunge mkono kwa lengo la kuleta
mabadiliko,” amesema.
No comments:
Post a Comment