VETA KUADHIMISHA MIAKA 30 IKIJIPANGA KUTUMIA NJIA TOFAUTI YA UFUNDISHAJI - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Wednesday, March 5, 2025

VETA KUADHIMISHA MIAKA 30 IKIJIPANGA KUTUMIA NJIA TOFAUTI YA UFUNDISHAJI


NA MWANDISHI WETU

WAKATI Mamlaka ya Elimu na Mafunzo Stadi (VETA) yakiwa katika maadhimisho ya miaka 30 tangu kuanzishwa kwake, Serikali imekuja na makakati wa kujenga ushirikiano na wadau wengine ili kuleta tija kwa vijana wanapokuwa vyuoni.

 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Aldof Mkenda amebainisha hayo leo Machi 5, 2025 jijini Dar es Salaam wakati akizungumza wa waandishi kuhusu maadhimisho hayo yanayofanyika kuanzia Machi 8 hadi 21 mwaka huu.

Amesema mgeni rasmi katika maadhimisho hayo atakuwa Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa na yatafanyika katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam na kufafanua kwamba yatakuwa ya kipekee kutokana na taifa kusherehekea mchango madhubuti unaotolewa na VETA tangu kuanzishwa kwake unaowawezesha vijana kupata ujuzi unaowakwamua kiuchumi.

Amefafanua kwamba kwa sasa mpango wa Serikali, VETA kujenge ushirikiano wenye viwanda na wadau wengine, mchakato utakaosaidia vijana wanaojiunga na vyuo hivyo kupata mafunzo ya vitendo kupitia wadau hao.

Prof Mkenda ametolea mfano uwepo wa wataalamu mbalimbali wenye uwezo mkubwa wa ubunifu wa kazi zao ambao hawana elimu ya darasani, mfano mafundi nguo, Seremala, ujenzi ambao wakitumiwa vizuri wanaweza kuwa msaada mkubwa kwa taifa.

“Tutawatumia hawa kufundisha wanafunzi wetu jambo tunaloamini litasadia kuwapa wanafunzi wetu ujuzi wa moja kwa moja na wakitoa hapo watakuwa wameiva tayari kuingia katika soko la ajira na VETA kwa kuwatumia hawa mafundi itaondokana na ukosefu wa walimu,” amesema. Huku Kaulimbiu ya maadhimisho hayo ni Ukuzaji Stadi na Ubunifu kwa Maendeleo ya Jamii na Taifa’.

 

Waziri Mkenda amesema shughuli mbalimbali zitafanyika katika kuelekea kwenye kilele cha maadhimisho hayo, ikiwemo kutoa huduma kwa jamii, kuendesha maonesho ya teknolojia na ujuzi, pamoja na kutoa tuzo na vyeti vya heshima kwa watu mbambali kwa mchango wao katika shughuli za maendeleo ya Ufundi Stadi nchini.

 

Amesema mwaka huu wataadhimisha miaka 30 ya VETA ambayo ilianzishwa kwa Sheria ya Bunge mwaka 1994 na kuanza kazi rasmi mwaka 1995. Kabla ya VETA kulikuwa na Idara ya Mafunzo na Majaribio ya Ufundi Stadi (NVTD) katika Wizara ya Kazi na Ustawi wa Jamii ambayo ilianzishwa mwaka 1975.

Amesema kwa kipindi cha miongo mitatu ya VETA imeendelea kuwa mstari wa mbele katika kuwajengea Watanzania uwezo wa kujiajiri, kuajiriwa, na kuchangia katika kukuza uchumi wa nchi.

 

Aidha amesema kuwa VETA imekuwa na mafanikio na kuwa taasisi muhimu inayochangia rasilimali watu yenye ujuzi inayohudumu katika sekta mbalimbali, ikiwemo Viwanda, Kilimo, Ujenzi, Teknolojia, Nishati na huduma na Utalii.

 

“Maadhimisho haya ya miaka 50 ya utoaji elimu na mafunzo ya ufundi stadi pamoja na miaka 30 ya VETA yanakuja wakati Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameagiza kukamilishwa ujenzi wa vyuo vya VETA vya hadhi ya kimkoa, katika mikoa yote ambayo haina vyuo hivyo kuanzia ngazi ya wilaya.

 

Amesema sasa VETA inakamilisha ujenzi wa chuo chenye hadhi ya Mkoa cha VETA kwa Mkoa wa Songwe na tunaendelea na ujenzi wa vyuo 64 katika wilaya 64 ambazo zilikuwa hazina vyuo hivyo.

 

“Nitumie fursa hii kuwakaribisha wadau wote katika maadhimisho haya yanayoendelea nchini na upekee katika kilele cha yatayofanyika jijini Dar es Salaam ili tujionee na kujadili umuhimu wa elimu na ujuzi kulingana na mabadiliko ya Sera ya Elimu na Mafunzo yam waka 2014 toleo la 2023,” amesema Profesa Mkenda

  

No comments:

Post a Comment