MWENGE wa Uhuru 2026 umeanza kukimbizwa katika Mkoa wa Dar es Salaam ambapo katika Wilaya ya Ilala miradi 7 yenye thamani *52,088,900,245.72* imepitishwa na Mwenge wa Uhuru hakuna mradi uliokataliwa.
Aidha katika miradi hiyo Mwenge wa Uhuru umetembelea, umekagua, kuweka jiwe la msingi na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa kitega uchumi cha DDC Kariakoo, ujenzi wa barabara ya lami mtaa wa Lindi, ujenzi wa kisima cha Ilala kota, ujenzi wa kituo cha afya Mchikichini, ujenzi wa shule mpya ya sekondari kitunda relini, ujenzi wa kituo cha polisi Bonyokwa na Kikundi cha vijana Fighter wanaojishugulisha na usafirishaji wa abiria kwa kutumia pikipiki.
Mwenge wa Uhuru 2026 leo April 14, unaendelea Wilaya Kigamboni ambapo utatembelea, utakagua, kuweka Jiwe la msingi na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo.








No comments:
Post a Comment