Jacob akiwa ndani ya hifadhi ya Ngorongoro,hifadhi iliyojaa kila aina ya wanyama siku hiyo aliamka asubuhi kuelekea kwenye majukumu yake.
Akiwa porini alikutana na pundamilia,alipowaangalia wale pundamilia walikuwa wamekaa mkao wa tahadhari,Jacob machale naye yakamcheza akaanza kutembea kwa tahadhari.
Mara paaa,kutupa jicho umbali wa mita tatu simba jike yupo mbele yake,alichofanya Jacob ni kumuangalia usoni simba yule,wote wawili wakawa wanaangaliana.
Jacob alimuangalia simba na simba naye alimuangalia Jacob,Jacob alipomuona simba hachezeshi masikio wala mkia akajua simba hajakasirika.
Kilichofuata Jacob akawa kila baada ya sekunde kadhaa anarudi nyuma kidogo kidogo mpaka akafika umbali wa mita 40 huku simba akiwa amesimama anatafakari la kufanya,hatimaye Jacob akajiokoa.
Karibu Ngorongoro uone maajabu.








No comments:
Post a Comment