KIDUME KILIVYOMPIGA SHERE SIMBA - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Tuesday, June 23, 2026

KIDUME KILIVYOMPIGA SHERE SIMBA


Jacob Lekumbere,Ofisa Utalii kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro hatosahau siku alipotumia mbinu za kimedani kumkwepa simba aliyetazamana naye uso kwa uso.


Jacob akiwa ndani ya hifadhi ya Ngorongoro,hifadhi iliyojaa kila aina ya wanyama siku hiyo aliamka asubuhi kuelekea kwenye majukumu yake.


Akiwa porini alikutana na pundamilia,alipowaangalia wale pundamilia walikuwa wamekaa mkao wa tahadhari,Jacob machale naye yakamcheza akaanza kutembea kwa tahadhari.


Mara paaa,kutupa jicho umbali wa mita tatu simba jike yupo mbele yake,alichofanya Jacob ni kumuangalia usoni simba yule,wote wawili wakawa wanaangaliana.


Jacob alimuangalia simba na simba naye alimuangalia Jacob,Jacob alipomuona simba hachezeshi masikio wala mkia akajua simba hajakasirika.


Kilichofuata Jacob akawa kila baada ya sekunde kadhaa anarudi nyuma kidogo kidogo mpaka akafika umbali wa mita 40 huku simba akiwa amesimama anatafakari la kufanya,hatimaye Jacob akajiokoa.


Karibu Ngorongoro uone maajabu.





No comments:

Post a Comment