KITABU CHA AFRIKA MAGUFULI NA BADILIKO ‘AFRICAN MAGUFULI AND CHANGE’ CHAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Sunday, August 13, 2023

KITABU CHA AFRIKA MAGUFULI NA BADILIKO ‘AFRICAN MAGUFULI AND CHANGE’ CHAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM


NA MWANDISHI WETU

WATANZANIA wanatakiwa kuamiani kuwa uongozi wa Dk Samia Suluhu Hassan auwezi kutenganishwa na wa hayati Dkt. John Magufuli na ndio sababu inayofanya miradi ya kimakakati kuendelea kutekelezwa kikamilifu.

Mathias Kabadi ambaye ni Mtanzania wa kwanza kuandika kitabu kuhusu hayati Magufuli, ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa kitabu cha pili ambacho kimetungwa na Prof. Malango Chintheng kutoka Chuo cha Hebron (UHB), Lilongwe nchini Malawi.

“Rais Dkt Samia, ni zao la hayati Dkt. Magufuli hivyo uwezi kuwatenganisha ndio maana  miradi iliyoanzishwa katika uongozi wake inaendelea kutekelezwa ikiwamo Bwawa la Mwalimu Nyerere, Standard Gauge Railway (SGR), Fly Overs ya Chang’ombe na hakuna ambao umesimama na itakamilika.

“Awali mwaka 2020 niliandika kitabu kuhusu hayati Magufuli kinachoitwa 'MJUE DKT. JOHN POMBE MAGUFULI', kuna baadhi ya watu waliamini ni kutokana na kutoka naye ukanda mmoja au sababu ya ukabira lakini mwaka huu, ametokea mtu mwingine tena kutoka nje ya nchi ameandika kitabu kingine na leo tunakizindua,” amesema.


Amesema kuwa Dkt Magufuli ataendelea kuandikwa kutokana uongozi wake kugusa maisha ya watu hususan masikini na aliamini Afrika si masikini kutokana na rasilimali ilizonazo.

Naye mwandishi wa kitabu hicho ambacho ni cha pili kuandika kuhusu hayati Magufuli na kuzinduliwa jijini Dar es Salaam Agosti 12, 2023 Prof. Malango Chinthenga kutoka Chuo cha Hebron nchini Malawi, amesema ametumia muda wa miaka sita kukusanya taarifa mbalimbali zinazomuhusu, Dkt Magufuli, katika uongozi wake ambao umeleta chachu na mabadiliko makubwa kwa Bara la Afrika.

Katika kitabu hicho Prof. Chinthenga anaelezea namna ambavyo Afrika inaweza kuendelea na hatua ambazo Tanzania ilipiga chini ya uongozi wa Rais hayati John Pombe Magufuli  kiuchumi na kiuongozi.

Kwa mara ya kwanza kitabu hicho kilizinduliwa siku chache zilizopita jijini Mwanza chini ya usimamizi wa Chuo  cha St. Augustine.

Pia mgeni rasmi katika uzinduzi wa kitabu hicho, Padri Stephano Musomba ambaye alimwakilisha , Askofu Mkuu wa Katoliki Jimbo Kuu la Dar e Salaam, Thaddeus Ruwa'ichi, amesema kuwa elimu ambayo wamepata watanzania imeathiriwa kutokana na kutaka kufanyiwa kila kitu.

Amesema kuwa wapo wanaotaka waitwe Prof, Dkt, bila kuufanyia kazi na kusistiza kinachotakiwa kuangaliwa kwa makini ni mila, malezi kwa vijana kwa maana wengi wao wanapenda kulelewa hali inayosababisha hata ndoa nyingi kutodumu.

 “Haiwezekani mtu wa nje anaamua kuandika kitabu kuhusu mtu wetu, sisi tunakwama wapi?, inawezekana ni kutokana na dharau zetu,” amesema.

Ameongeza kuwa kitabu hicho kinachoitwa Africa Magufuli and Change (Africa Magufuli na Badiliko) ni vema kisomwe na si kuweka kabatini kwa maana kinaweza kuleta mabadiliko ya kuishi vema kwani mfumo wa maisha yetu haupo kama Ulaya, kwa watanzania ni shirikishi.



No comments:

Post a Comment