Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Dk.Samia Suluhu Hassan akizungumza kwenye ufunguzi wa Kikao Kazi kwa Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma kilichoandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina kwa kushirikiana na Jukwaa la Wakuu wa Taasisi za Umma, kilichofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa AICC Jijini Arusha tarehe 19 Agosti, 2023.
..................................................
NA MWANDISHI WETU, ARUSHA
RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan ameridhishwa na
mabadiliko yanayoendelea Bohari ya Dawa ( MSD) na kuwataka waendeleee kuchapa
kazi.
Rais Samia amesema hayo Jumamosi Agosti 19,
2023 jijini Arusha wakati akifungua kikao kazi cha wenyeviti wa bodi na taasisi
za umma.
Rais Dk.Samia akiwa amemsimamisha Mkurugenzi wa MSD, Mavere Tukai amesema taasisi hiyo ni kati ya mashirika yaliyibadilika na matumaini yake itakwenda kufanya vizuri hasa katika mfumo wa uuzaji wa Dawa Afrika kwa kuwa na soko kubwa hususani kwa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara (SADC).
CREDIT, HABARI ZAJAMII





No comments:
Post a Comment