JESHI LA POLISI LISIKAE KIMYA KWA WANASIASA WANAOMTUKANA RAIS MITANDAONI - STEVE NYERERE - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Monday, March 11, 2024

JESHI LA POLISI LISIKAE KIMYA KWA WANASIASA WANAOMTUKANA RAIS MITANDAONI - STEVE NYERERE

Steve Nyerere (wa pili kulia)ambaye ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao akizungumza na waandishi wa Habari.
NA MAGENDELA HAMISI

TAASISI ya Mama Ongea na Mwanao, imewataka wanasiasa kuacha kufanya siasa za matusi na kumkashifu Rais, Samia Suluhu Hassani.

Pia amelitaka Jeshi la Polisi kutokaa kimya kwa wanasiasa wanaomtukana Rais mitandaoni kwani wanatakiwa kukamatwa na kuhojiwa na wakipatikana na hatia wapandishwe kizimbani wakajibu tuhuma zao.

 Hayo yamezungumza leo Machi 11, 2024 jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa taasisi hiyo, Steve Nyerere na kusisitiza hawezi kukaa kimya kuona Rais Samia, akitukanwa na baadhi ya wanasiasa wanaofanya siasa chafu.

 Pia ameshangazwa na kuona kijana ambaye ametusi Rais akiwa bado hajakamatwa na vyombo vya Ulinzi na Usalama huku chama chake cha siasa kikiwa tayari kimefukuza uanachama.

“Huyu mtu nguvu ya kumtukana rais anaitoa wapi na yuko nyuma ya nani na kwa nini hadi leo hajakamatwa,” alihoji Steve Nyerere.

Ameongeza kuwa ifike wakati baadhi ya wanasaisa wakachunga kauli zao kabla ya kusema ili kujenga amani na utulivu nchini.

“Tunalaani kitendo hicho kwa mtu huyo kumtukana Rais mitandaoni na tunatoa wito kwa wanasiasa kufanya siasa za hoja bila matusi ambayo hayana afya kwenye siasa,” amesema.

Pia amewataka watu ambao wapo karibu na Mama (Rais) kuhakikisha wanakuwa imara katika kuwadhibiti na kutokaa kimya kwa wanasiasa wanaomtukana rais mtandaoni.

 

“Mlio karibu na Mama, msikae kimya mama anapotukanwa, mnatakiwa kujibu, hakuna mtu anaweza kukaa kimya huku mama yake anatukanwa, haiwekani,” amesema.

Wakati huo huo, Steve Nyerere ametoa wito kwa vijana kutumia vema mitandao kwa ajili ya kujiongezea kipato na si kufanya mambo ambayo yatawafanya kuwa masikini.

No comments:

Post a Comment