TAWA: MIAKA MITATU YA RAIS SAMIA,TUMEONGEZA WATALII, TUMEIMARISHA ULINZI WA TEMBO - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Monday, March 18, 2024

TAWA: MIAKA MITATU YA RAIS SAMIA,TUMEONGEZA WATALII, TUMEIMARISHA ULINZI WA TEMBO

Kamishna wa Uhifadhi TAWA, Mabula Nyanda akizungumza leo Machi 18, 2024 akielezea mafanikio yao kwa kipindi cha miaka mitatu.


NA MAGENDELA HAMISI

MAMLAKA ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) katika kipindi cha miaka mitatu ya Rais Samia Suluhu Hassan, inajivunia kutekeleza majukumu yao kiufasaha ikiwemo kuongeza watalii baada ya kuwezeshwa kifedha.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Machi 18, 2024 katika mkutano na wahariri na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari nchini, Kamishna wa Uhifadhi TAWA, Mabula Nyanda amesema kwa katika kipindi hicho wamefanikiwa kuongeza idadi ya watalii.

“Mwaka 2020/21 tulianza na watalii 37, 684 na mwaka 2022/23 tumepata watalii 166, 964 kwa mwaka huu hadi kufikia Feb tumefanikiwa kuingiza watalii 116, 529 na tutakapomaliza mwaka tunaratajia kufikia malengo makubwa zaidi, amesema.

“Na yote hayo yamechangiwa kwa asilimia kubwa na Rais wetu, Dkt Samia Suluhu Hassan kutuwezesha kifedha na filamu ya Rolay Tour kufanya kimataifa jambo ambalo limesadia kuitangaza Tanzania na watalii kumiminika kwa wingi, amesema   

Amesema kuwa tofauti na watalii kuja nchini, pia meli kubwa za kitalii mwaka 2020/21 ziliingia nne na mwaka 2023/ 24 zimefanikiwa kuingia meli nane jambo ambalo ni mafanikio makubwa kwa TAWA na Serikali kwa ujumla.

Ameongeza kuwa mafanikio mengine baada ya kuwezeshwa na Rais Dkt Samia katika kipindi cha miaka mitatu tangu aingie madarakani ni kuhimalisha ulinzi wa rasilimali, wanyamapori na malikale.

Amefafanua kuwa kwa kupindi hicho cha miaka mitatu ya Rais Samia, wamefanikiwa kupunguza ujangili wa tembo kwa asilimia 83, ambapo kwa mwaka 2021/22 kuwa na mizoga sita hadi kufikia mizoga mitatu kwa mwaka 2023/24.

Ameongeza kuwa yote hayo yamesababishwa na kupata vitendea kazi vinavyosaidia kuhimilisha mtandao wa kitelejinsia wa kupata taarifa mbalimbali ujangili inayozeshwa ufungwaji wa visukuma mawimbi kwa tembo.

Pia TAWA katika kipindi cha miaka mitatu, wanajivunia kupunguza migogoro ya mipaka na wananchi katika mapori ya Akiba saba na moja likiwa katika hatua za mwisho kukamilika ili kuweka hali shwari kwenye jamii.

Kamishna Mabula amesema migogoro ambayo tayari wameimaliza ni katika mapori saba ambayo ni Mkungunero, Swagaswaga, Igombe, Wamimbiki, Mpanga Kipengere, Selous na Liparamba huku Kilombero likiwa katika hatua za mwisho kumalizia mgogoro.

Katika utatuzi wa migogoro kwenye eneo la ekari 103, 544.48 ambalo limemegwa kutoka hifadhi na kuwapa wananchi kwa ajili ya shughuli za kiuchumi, serikaloi kupitia TAWA, inaendelea kulipa fidia kaya 45 zilizo katika pori la Akiba Mkungunero.

Ameongeza kuwa anaamini hali itaendelea kuwa tulivu kutokana na kushirikiana na jamii vema na kuchangia miradi ya maendeleo katika maeneo husika ikiwemo ujenzi wa masoko, madarasa.

Katika hilo Kamishna Mabula amesema katika kipindi cha mwaka 2021/24, wamechangia katika miradi ya jamii shilingi milioni 193 ambapo kwenye ujenzi wa soko la samaki katika mji wa Ifakara Kilombero wametumia mil 66.

Pia wamenunua mashine mbili za kusaga mkoani Mara na kuchangia mil 10 katika ujenzi wa Zahanati na vyumba vya madarasa Mwibara, ikiwemo mil 20 katika ujenzi wa Zahanati ya Bungo ya wilayani Korogwe mkoani Tanga.

Pia kwenye ujenzi wa vyumba vya madarasa, ofisi za walimu na ununuzi wa madawati katika Shule ya Msingi Usinge iliyoko Kaliua mkoani Tabora wametoa sh. mil 50  na madawati 100 wameyatoa wilayani Bunda.

Katika mafanuikio yote haya ambayo tumepata kwa kweli tunamshukuru Rais Samia kwa kutuwezesha, bila yeye tungekuwa na wakati mgumu kufikia hapo, pia katika kipindo hicho tumefanikiwa kununua magari 60, meli za doria tisa na mashine ya uchimbaji visima vya maji ambayo yanasaidia kwa ajili matumizi ya wafanyakazi wetu na raia kwa ujumla, tunamshukuru sana Rais Samia., amesema

 






No comments:

Post a Comment