WAANDISHI WA HABARI MITANDAONI KUKUTANA NA WAZIRI MKUU - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Saturday, May 18, 2024

WAANDISHI WA HABARI MITANDAONI KUKUTANA NA WAZIRI MKUU

                                                                                                      (PICHA KWA HISANI YA MTANDAO)

NA MAGENDELA HAMISI

JUMUIYA ya Waandishi wa Habari wa Mtandaoni (JUMIKITA) imepanga kuwakutanisha wana mahudhui hayo na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa kwa lengo la kujadili mapinduzi ya tasnia hiyo kupitia mitandao ya kijamii

 

 

Hayo yamebainishwa leo Mei 18, 2024 jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa JUMIKITA, Shabani Matwebe na kufafanua kuwa waandishi zaidi ya 800 wa mtandaoni watakutana na Waziri Mkuu Majaliwa Jumatatu katika ukumbi wa Maktaba wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

 

“Jumikita tunaona kwamba kuna haja ya kuzungumza na wadau mbalimbali wa mitandao ya kijamii na kujadili kwa pamoja tukiwa na Waziri Mkuu mapinduzi yaliyopo katika tasnia ya habari na utangazaji kupitia mitandao ya kijamii na changamoto zilizopo ili kupata njia ya sahii ya kufikia mafanikio,” amesema.

 

Ameongeza kuwa mkutano huo utawajumuisha waandishi kutoka kona zote za Tanzania kupitia kandao zao, watu maarufu na Shirikisho la Serikali ya Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Tanzania (TAHLISO) ikujumuisha wanafunzi ambao wamo katika mahudhui ya habari mtandaoni.

 

Ameweka wazi kuwa katika mkutano huo utaambana na kuadhimisha miaka mitatu ya JUMIKITA itakayotoa fursa ya kuangalia changamoto zilizoko na kuzitatua jambo litakalosaidia kufikia mafanikio yanayohitajika kupitia tasnia hiyo.

 

Ameongeza kuwa baadhi ya mambo machache watakayowasilisha kwa Waziri Mkuu, Majaliwa ni namna wanavyohitaji kupewa nafasi katika mihaliko katika kuchukua habari kwenye taasisi mbalimbali nchini kama inavyofanyika katika vyombo visivyokuwa vya mitandaoni.

 

No comments:

Post a Comment