NDOA NYINGI ZINAZOVUNJIKA NI ZA VIJANA: MCHUNGAJI DKT. MKAMA - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Sunday, June 2, 2024

NDOA NYINGI ZINAZOVUNJIKA NI ZA VIJANA: MCHUNGAJI DKT. MKAMA

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Assembles Of God (TAG), Ilala Mission, Dkt Titus Mkama. (PICHA KWA HISANI YA MTANDAO MTEZA BLOG)

NA MWANDISHI WETU

IMEELEZWA kuwa vijana ndio wanaovunja ndoa tofauti na wazee na hiyo inatokana na wengi wao kuingia katika mahusiano hayo kwa tamaa za mafanikio bila kuchunguza kwa kina tabia za mwenza wake.

Hayo yamesemwa na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Assembles Of God (TAG), Ilala Mission, Dkt Titus Mkama Mei 28 mwaka huu wakati akizungumza na Waandishi wa Habari ofisini kwake Ilala jijini Dar er es Salaam.

“Shida kubwa ambayo ipo ni vijana wengi kuingia katika ndoa bila kuwa na hofu ya Mungu na kuvutwa na tamaa ya mafaniko ya uchumi ya mmojawapo na inapokuja kuwa tofauti migogoro inapoanza.

“Tunapotaka kuwafungisha ndoa tunawaambia kabisa ndoa huwa haivunjiki na biblia inakataa kuvunjika kwa ndoa ila baada ya kufungishwa na kuona baadhi ya vitu haviendi sawa hawataki kabisa kusikia kitabu cha dini kinasema nini wanasimamia msimamo wa kuvunja ndoa tu.

“Na hapo inakuwa ngumu kuwarejesha katika ndoa tofauti na wazee walio kwenye ndoa wengi wao wakipata changamoto ukizungumza nao wanarejea katika mstari tofauti na vijana wa dot com,” amesema.

Ameongeza kuwa kinachotakiwa kwa vijana wanaotaka kuingia katika maisha ya ndoa kabla ya kuchukua uamuzi huo wanatakiwa kumuomba Mungu ili awape mtu sahihi kwa ajili ya ndoa .

Ameweka wazi kuwa kanisa lake la Assembles of God Tanzania (TAG), Ilala Mission tangu lianzishwe mwaka 1973 limefungusha ndoa zaidi ya 400  na anashukuru kuona ndoa nyingi za zamani zikiendelea kudumu tofauti na za sasa.

No comments:

Post a Comment