TCB YATOA MSAADA WA MABATI 250 KWA HALMASHAURI YA UYUI - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Wednesday, September 18, 2024

TCB YATOA MSAADA WA MABATI 250 KWA HALMASHAURI YA UYUI




NA MWANDISHI WETU

BENKI ya TCB imekabidhi mabati 250 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui mkoani Tabora, ikiwa ni sehemu ya juhudi zake za kusaidia maendeleo na kurudisha shukrani kwa jamii.

 

 Hafla ya kukabidhi mabati hayo imefanyika leo wilayani humo na  imeongozwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma, Chichi Banda, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, wananchi na wawakilishi wa benki hiyo mkoani Tabora.

 

Akizungumza katika hafla hiyo, Banda, amesema wanayofuraha kutoa msaada huo ikiwa ni sehemu ya kurudisha shukrani kwa jamii na wanaamini kwamba ni kichocheo cha kuboresha maendeleo wilayani humo.

 “Tunafurahia kutoa mabati haya kwa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui, lengo letu ni kusaidia katika miradi ya maendeleo ambayo itaboresha maisha ya wananchi.

 

“Tunaamini kuwa rasilimali hizi zitakuwa na manufaa makubwa katika ujenzi wa miundombinu na huduma za jamii, amesema.

 

Mabati hayo yamepangwa kutumika katika ujenzi wa shule, vituo vya afya, na nyumba za makazi na kusaidia kuboresha mazingira ya maisha na elimu kwa jamii.

 

 Halmashauri ya Wilaya ya Uyui, inasisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi ili kufanikisha maendeleo endelevu.

 

“Tunawakaribisha wananchi kushiriki katika miradi hii, na tunatoa shukrani zetu za dhati kwa Benki ya TCB kwa mchango wao mkubwa. Huu ni mfano mzuri wa namna sekta za Serikali zinavyoweza kusaidia katika maendeleo ya jamii,” amesema Venance Protas (MB).

 

Hafla hiyo ilikamilika kwa burudani mbalimbali na wananchi wakitoa shukrani zao kwa benki ya TCB kwa kutoa msaada huo ambao wanaamini utaleta tija katika kuleta maendeleo ya Halmashauri ya wilaya hiyo kwa kusaidia kuboresha huduma na maisha ya wananchi wa Uyui kwa ujumla.



No comments:

Post a Comment