JAMII YATAKIWA KUWAAMINI NA KUWAPA NAFASI ZA UONGOZI WASICHANA - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Thursday, October 10, 2024

JAMII YATAKIWA KUWAAMINI NA KUWAPA NAFASI ZA UONGOZI WASICHANA

 


NA MAGENDELA HAMISI

WITO umetolewa kwa jamii kutoa nafasi kwa wasichana kushika nafasi za uongozi kwa kuwa wanauwezo kuleta mabaadiliko chanya na kuchangia maendeleo ya nchi.

Hayo yamebainishwa leo jijini Dar es Salaam na Jane Sembuche ambaye ni Mkurugenzi Mkazi wa Plan International wakati akihitimisha Kampeni ya Chukua Hatamu  'Girls Takeover' ambapo wasichana zaidi ya 40 wameshiriki katika hafla hiyo.

Kampeni hiyo, inatekelezwa na shirika hilo ikishirikiana na Serikali lengo likiwa ni kuhakikisha mtoto wa kike anatimiza ndoto zake ikiwa atapatiwa fursa ya uongozi katika nyanja mbalimbali ikiwemo kwenye siasa.

"Shughuli ya namna hii, tunaifanya kila mwaka Oktoba 11na na inakwenda pamoja na kuheherekewa siku ya mtoto wa kike duniani kote na tunaiita 'Girls Takeover' kwa tafsiri ya Chukua Hatamu ambayo ni mahususi kumhamasisha msichana kufanya jitihada na kujituma pindi anapopewa nafasi ya uongozi Kwa maana tunaamini anaweza," amesema

Ameongeza kuwa Kwa namna wasichana wanavyokuwa na ujasiri ikiwa watahamasishwa wataweza kuwa viongozi wazuri na kuleta maendeleo stahiki katika jamii na mifano iko mingi na ya kuigwa kwa jinsi hiyo kufanya vema na kinachotakiwa na kuwapa hamasa kuwa wanaweza.


Akizungumzia uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba mwaka huu Mkurugenzi huyo Mkazi wa Plan International Tanzania amesema kuwa pamoja na shirika hilo kutekeleza Kampeni ya Girls takeover lakini pia lina kampeni nyingine ya "Sikia Sauti zetu " ili kuwezesha sauti za wasichana sehemu mbalimbali wanahamasika kuzungumza  nakuleta changamoto zao katika sehemu husika.


" Tunaamini wanaendelea kukuzika katika uongozi kuanzia ngazi za jamii na kupata uzoefu kwahiyo nikuhamasisha wote ambao wana uwezo wasifikirie kama kitu kigumu,wajitokeze kuwania nafasi hizo" amesisitiza.

Kwa upande wake Mkurugenzi msaidizi idara ya Maendeleo ya watoto Wizara ya Maendeleo ya Jamii ,Jinsia, Wanawake na Makundi maalumu Bw.Mathias Haule amesema kuwa kampeni ya Girlstakeover imeenda sambamba na kauli mbiu ya siku ya mtoto wa kike kimataifa inayosema "Mtoto wa kike na uongozi,tumshirikishe wakati ni Sasa" ,hivyo serikali kwa kushirikiana na Plan International itahakikisha watoto wa kike wanapata nafasi za uongozi katika maeneo mbalimbali hasa wakiwa mashuleni.


No comments:

Post a Comment