MADINJ YAJENGA UWANJA WA MPIRA CHUNYA - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Friday, October 10, 2025

MADINJ YAJENGA UWANJA WA MPIRA CHUNYA



NA MWANDISHI WETU

SHUGHULI za madini katika Mkoa wa kimadini Chunya mkoani Mbeya zimechangia ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu wa kisasa wilayani humo, kupitia michango ya wadau mbalimbali wa maendeleo wakiwemo wa madini.

Akizungumza katika mahojiano maalum na timu ya Madini Diary kutoka Wizara ya  Madini,  Mjumbe wa  Kamati ya Maandalizi ya Ujenzi wa Uwanja  huo ambaye pia ni  Mkurugenzi  wa  KenGold Sports Club, Keneth Mwakyusa amesema  kuwa, kujengwa kwa uwanja huo kunatokana na jitihada  zilizofanywa na  Halmashauri ya Chunya  kwa kushirikiana na wadau  mbalimbali wakiwemo wa  sekta ya madini.

"Tunaweza kusema mapato ya madini pia yamehusika katika ujenzi wa uwanja kwa sababu wadau  waliochangia wapo pia wa madini  ambao  wametumia fedha zilizotokana na  na shughuli za madini lakini wapo na wadau wengine nje ya madini na usimamizi  mkuu  umefanywa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chunya akisaidiana na kamati ya ujenzi,’’ amesema.

Ameongeza kwamba, uwanja huo utatumiwa na timu za Chunya ikiwemo KenGold na siku za usoni  wanatarajia timu kubwa za Yanga,  Simba, Azam na nyingine .

Amesema uwepo wake  ukitarajiwa kuchochea ukuaji wa sekta nyingine  kama hoteli, usafiri, chakula na nyingine na kuongeza kwamba hatua iliyofikiwa hivi sasa ni uwekaji wa nyasi bandia.

Akizungumzia mwenendo wa timu ya Kengold amesema timu hiyo inaendelea na mazoezi  na  wana imani itarejea ligi kuu kwenye msimu ujao na kuwataka wadau wa michezo nchini wakiwemo wananchi wa Chunya kuendelea kuiunga mkono timu hiyo.

Naye, Fundi wa uwanja huo Msafiri Napanja amesema kazi inayoendelea  hivi sasa ni uwekaji wa nyasi bandia iliyopangwa kufanyika ndani ya siku 30 huku maendeleo ya ujenzi wa uwanja yamefikia asilimia 85.

Awali, akizungumza na timu hiyo ya Madini Diary, Afisa Madini Mkoa wa Kimadini Chunya Mhandisi Laurent Mayalla amesema kwamba mchango wa sekta ya madini wilayani Chunya umeyagusa maeneo mengi ikiwemo ya michezo kutokana na ujenzi wa uwanja  huo.




No comments:

Post a Comment