SERIKALI YATENGA MAENEO YA KUHIFADHI WAGONJWA WA EBOLA - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Thursday, October 13, 2022

SERIKALI YATENGA MAENEO YA KUHIFADHI WAGONJWA WA EBOLA

 
Na Pamela Mollel,Arusha

Serikali Mkoa Arusha imeanza mkakati maalumu wa kutenga maeneo ya kuhifadhi wagonjwa wa ebola endapo watatokea kutokana na kuripotiwa ugonjwa huo kuwepo nchi jirani

Akizungumza katika kikao cha afya ya msingi kilichoshirikisha Viongozi na wadau wa afya jijini Arusha Mkuu wa Mkoa Arusha John Mongella amewataka wataalamu wa afya kutoa elimu kwa wananchi juu ya ugonjwa wa Ebola na namna ya kuchukua tahadhari

Mongella alisema kuwa wananchi wakipewa elimu ya kutosha itasaidia wao kuchukua tahadhari kabla ya hatari

"Hii elimu pelekeni vijijini wananchi huko hawana uelewa juu ya uwepo wa ugonjwa wa hatarii wa Ebola "alisema Mongella

Kwa upande Mganga Mkuu wa mkoa wa Arusha Dkt Sylvia Mamkwe alisema kuwa lengo la kikao hicho ni kujadili kwa kina namna ya kuchukua tahadhari endapo ugonjwa huo utaingia nchi

Amesema kwa sasa hakuna mgonjwa aliyeripotiwa kuwa na ugonjwa huo hatari na serikali inaendelea kuchukua hatua namna ya kukabiliana nao

Aidha mamkwe alisema jumla ya watumishi 122 wa afya wameandaliwa kutoa elimu katika maeneo mbalimbali vijijini

"Kwa sasa tunakabiliwa na changamoto ya vifaa ila serikali inapambana kuhakikisha inapata vifaa vya kukabiliana na ugonjwa huo"alisema Mamkwe

Dalili za ebola ni kutoka kwa damu maeneo mbalimbali ya mwili kama vile masikioni,mdomono,puani

Mganga mkuu wa mkoa wa Arusha Dkt Sylvia Mamkwe akizungumza na vyombo

Viongozi na wadau wa sekta ya afya jiji la Arusha wakiwa katika kikao maalum cha kujadili namna ya kuchukua tahadhari endapo ugonjwa huo utaingia nchini


No comments:

Post a Comment