ACT WAZALENDO YATOA MAONI KWA SERIKALI NAMNA YA KUKABILIANA NA UPATIKANAJI MAFUTA YA PETROL NA DISELI - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Thursday, August 17, 2023

ACT WAZALENDO YATOA MAONI KWA SERIKALI NAMNA YA KUKABILIANA NA UPATIKANAJI MAFUTA YA PETROL NA DISELI




NA MAGRETHY KATENGU

 

CHAMA cha ACT Wazalendo Chafafanua mambo matano ambayo Serikali inapaswa  kuyachukulia hatua ili kukabiliana na changamoto za upatikanaji wa mafuta ya Petroli na Diseli nchini pia kupanda bei. 

Akizungumza na waandishi wa habari leo  jijini Dar es Salaam Waziri Kivuli wa Sekta ya Nishati wa Chama hicho Isihaka Mchinjita amesema hivi karibuni mafuta hayo yamepanda bei hivyo wameona hawawezi kukaa kimya wakaona watoe ushauri serikali  hatua  zinazopaswa kuchukua ni ikiwemo , Serikali kuweka msisitizo wa kupunguza matumizi ya mafuta ya Petroli na Diseli kwa kutumia nishati mbadala ya Gesi asilia kuanzia kwenye magari ya serikali na mabasi yaendayo mkoani. 

"Inawezekana kwa kuchukua hatua kadhaa za haraka ikiwemo magari yote ya Serikali kuanza kutumia Gesi asilia (CNG) na bohari zote za Serikali (GPSA) zifungwe mitambo ya kujazia gesi asilia (CNG) Vilevile, mabasi ya mwendokasi nayo yabadilishwe mfumo na yaanze kutumia gesi asilia ,magari ya abiria ya mikoani (mabasi) yote yafungwe mfumo wa kutumia mitungi ya Gesi asilia (CNG), ili kupunguza kutumia fedha nyingi za  kuagiza bidhaa za mafuta,” amesema Mchinjita.

Mchinjita amefafanua kuwa hivi karibuni wanaoagiza mafuta nje ya nchi wanakumbana uhaba wa dola kwani ndiyo fedha inayotumika kuagizia mafuta hivyo  ni vyema Serikali ianze kupunguza matumizi ya dola za Kimarekani kwa Benki Kuu kuruhusu wanunuzi wa mafuta kulipia kwa shilingi kisha benki hiyo ndio iwalipe wanunuzi wa nje kwa dola za Kimarekani ili kuwarahisishia wafanyabiashara ya mafuta wasihangaike kutafuta dola.

Amesema Tatu, hatua nyingine, ni kuhakikisha Serikali inadhibiti mahitaji ya dola kwa kuhakikisha matumizi yote ya ndani yanafanywa kwa shilingi ya Tanzania nne, kuongeza mauzo ya bidhaa za kilimo nje ikiwemo kuongeza thamani ya mazao

Awali akizungumzia kuhusu hali ya upatikanaji wa mafuta ya petroli na diseli, amesema katika uchambuzi wa Chama hicho  walioufanya Agosti 2, 2023 ulijikita zaidi katika kuangalia tatizo la kupanda kwa bei za mafuta na sababu zilizopelekea kupaa huko na walitoa mapendekezo yao ili kushusha bei hizo kwani   hivi karibuni wamekuwa wakifuatilia kwa karibu zaidi juu ya hali ya upatikanaji wa mafuta nchini na kwa mujibu wa utafiti wao wamebaini kuwepo kwa changamoto ya upatikanaji wa mafuta katika hifadhi ya mafuta bandarini (Dar es Salaam).

Amebainisha kwamba changamoto ya upatikanaji wa mafuta imepelekea waagizaji wa mafuta hususani kwa waagizaji wadogo kuchelewa kupata mzigo kutoka bohari za bandari ya Dar es Salaam kwani awali iliwachukua siku 1 tu sasa inachukua siku 3 hadi 4 kupata mafuta na kupakia katika Bohari za Dar es salaam jambo linalopelekea uhaba katika maeneo mengi.

“Hali katika bandari ya Mtwara imekuwa mbaya kwa mafuta ya petroli ambapo hayapatikani kabisa, jambo linaloplekea wauzaji wote waliokuwa wanachukua mafuta katika bandari ya Mtwara kulazimika kufuata Dar es Salaam,” ameeleza Mchinjita.

Ingawa wanafahamu uwezo wa nchi kuhifadhi mafuta ni wa mwezi mmoja, lakini tulikuwa tunaagiza mafuta kwa kutangulia miezi miwili hivyo kwa sasa mafuta yanayotumika ni yale yaliyoagizwa mwezi huu wa nane.

Kwamba sababu kubwa inayopelekea kuwepo kwa tishio la uhaba wa mafuta nchini ni kupungua kwa uwezo wa kuagiza mafuta kwa waagizaji wetu kutokana uhaba wa dola pia kupanda juu pia tangu mwezi Machi kutokana na uhaba wa dola waagizaji wamekuwa wakipunguza kiasi wanachoagiza.

Amesema hii ni kutokana na uhaba wa dola za marekani na kushuka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania kwa dola, jambo linalopelekea waagizaji kupoteza kiasi kikubwa cha fedha katika kubadilisha shilingi kwenda dola za marekani.

Amefafanua kuwa katika hali hii Serikali haipaswi kusubiria miujiza kukabiliana na changamoto hizi au kusubiri kutokea kwa athari kubwa zaidi ndio ichukue hatua za kunusuru ni hatari ya Serikali kutochukua hatua za haraka ni kupelekea kupandisha bei zaidi na kuongeza kiwango cha uhaba zaidi nchini.

Amesisitiza kuwa tatizo la mafuta upatikanaji na gharama zake linahitaji hatua za makusudi za Serikali.

Kwamba ni muhimu kwa Serikali kuuza nje bidhaa zinazotokana na kilimo badala ya kuuza malighaf pia kuweka vivutio katika sekta ya utalii kwa kuongeza matangazo na kuboresha miundombinu ya Utalii ili kuongeza idadi ya watalii maradufu ya idadi ya sasa. 

"Tukifika watalii Milioni 5 kwa mwaka, nchi yetu itapata fedha za kigeni mara tatu ya tunazopata sasa na kuongeza ajira nyingi kwa watanzania," ameeleza

 



No comments:

Post a Comment