KINANA: TUTAKWENDA KWENYE UCHAGUZI MKUU TUKIWA NA MAELEWANO MAKUBWA - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Tuesday, August 22, 2023

KINANA: TUTAKWENDA KWENYE UCHAGUZI MKUU TUKIWA NA MAELEWANO MAKUBWA

 


NA MAGENDELA HAMISI

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana, amewahakikishia Watanzania kuwa watakwenda kwenye Uchuguzi Mkuu ujao huku vyama shiriki vikiwa na maelewano makubwa.

 Pia amekiri kuwa licha ya nchi kuwa na uhuru wa kutosha wa kuzungumza lakini bado kuna kasoro kadhaa ambazo zinatakiwa kufanyiwa kazi ili kuondoa kelele za baaadhi ya watanzania katika utekelezaji wake.

 “Kuhusu demokrasia ukiacha miaka michache iliyopita kwa sasa ipo vizuri ndio maana watu wamekuwa na uhuru wa kutosha katika kuzungumza ingawa kila uhuru una mipaka yake na ndio inayofanya baadhi ya watanzania kulalamika katika usimamizi wa sheria,” amesema.

Kinana alitanabaisha hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa Mkutano Kitaifa wa Wadau, kujadili Hali ya Demokrasia nchini kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Katika Mkutano huo ambao umeandaliwa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), Pia Kinana alifafanua kwamba kabla ya kuanza kwa mchakato wa Katiba Mpya, Asasi za kiraia zitatoa elimu kwa Watanzania kupitia yaliyomo kwenye Katiba ya mwaka 1977 ili kutoa dira ya kukamilisha hilo kabla ya uchaguzi ujao.

 “Fungu ambalo limeandaliwa kwa ajili ya kutoa elimu kwa Watanzania litawezesha asasi za kiraia ili kufanikisha mchakato wa Katiba Mpya jambo litakalosaidia kwenda kwenye uchaguzi mkuu tukiwa na maelewano yatakayofanya uchaguzi kuwa huru na haki,” amesema . 

 Pia aliwasisitiza wajumbe wa mkutano huo kujadiliana vizuri changamoto zilizopo ili maadhimio yatakayopatikana yapelekwe serikalini haraka kwa ajili ya kufanyiwa kazi na kuondoa upungufu unaolalamikiwa.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Chama na NCCR Mageuzi, Joseph Selasin, ameshauri kwamba ni vizuri uchaguzi wa Serikali za Mitaa na ukasimamiwa na Tume ya Uchaguzi badala ya kusimamiwa na Tamisemi kama ilivyo sasa.

“Nakumbuka mwaka 1995 tulifanya uchaguzi vizuri kwa kuwa tume iliajiri wafanyakazi wake na wapinzani tukafanya vizuri sana kwa maana tulifanikiwa kupata asilimia 40 ya kura na baada ya hapo tukashuka kutokana na kuwa chaguzi ya upande mmoja ni ni vema michakato hii ikafanyika kwa haraka,” amesema.

 

 


No comments:

Post a Comment