SH. BIL 5 ZATENGWA NA MFUKO WA KUWEZESHA WASANII NA WAIGIZAJI MKOA WA MBEYA - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Tuesday, August 15, 2023

SH. BIL 5 ZATENGWA NA MFUKO WA KUWEZESHA WASANII NA WAIGIZAJI MKOA WA MBEYA

                     

AfisaUtamaduni Mkoa wa Mbeya Victoria Shao akizungumza katika kikao maalumu kilichowahusisha Wasanii, Waigizaji na waimbaji kilicho andaliwa na Wizara ya Utamadunim Sanaa na Michezo.

............................................................

NA MWANDISHI WETU, MBEYA

KIASI cha Shilingi Bilioni 5, zimetengwa na Mfuko wa Wizara ya Sanaa na Utamaduni ili kuwawezesha wasanii na waigizaji wa "Bongo Movie" wa Mkoa wa Mbeya.

Akizungumza katika kikao maalumu kilichowahusisha wasanii, waigizaji na waimbaji wa mikoa ya Mbeya na Songwe, Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa mfuko huo, Nyakaho Mahemba, amesema wizara imeanza kutoa fedha hizo kwa wasanii kuanzia Desemba 2022 na imelenga kukuza na kuendeleza kazi za wasanii kujiendesha kibiashara badala ya kuwa burudani pekee.

Mahemba amesema katika mpango wa Serikali ni kuongeza ajira na kuongeza mitaji kwa wasanii kupitia mafunzo na kuongeza ubora  wenye lengo la kukidhi soko la ndani na nje ya nchi.


Amefafanua kuwa wasanii wana uwezo wa kukopa mtaji kuanzia sh. laki 2 hadi sh. Mil 100 ili kufikia malengo na kwamba Mfuko wa Utamaduni unashirikiana na mabenki ili kuwezesha mikopo ya wasanii.

Afisa Mtendaji Mkuu, huyo ameendelea kusema kuwa tayari imeshatolewa mikopo kwa awamu mbili, Desemba 2022 na mkopo wa pili umetolewa Februari ambapo tayari  jumla ya sh. bil 1.077 kwa miradi 45 na hivyo kuzalisha ajira 88,750.


Kwa upande wake Afisa Utamaduni wa Mkoa, Victoria Shao, amesema mikopo hiyo ya wasanii itachangia ajira na kuwasaidia kuwainua kiuchumi ambapo wasanii,waimbaji,wabunifu wa kazi za mikono,waandishi wa kazi za kifasihi na wachoraji wanapaswa kuchangamkia fursa hiyo.

Shao amesema serikali itakuwa karibu na wasanii kwa maelekezo na elimu ya mikopo ili waweze kukopa kurejesha ili iweze kuwanufaisha wasanii wengine.



No comments:

Post a Comment