MADEREVA WASTAAFU WAHITAJIKA CHUO CHA FURAHIKA - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Monday, March 11, 2024

MADEREVA WASTAAFU WAHITAJIKA CHUO CHA FURAHIKA



NA MWANDISHI WETU

UONGOZI wa Chuo cha Ufundi Stadi cha Furahika chenye namba za usajili VET/DSM/PR/2021D169 ambacho kipo Buguruni Malapa – Ilala jijini Dar es Salaam, umesema kuwa wanawahitaji madereva wastaafu kwa ajili ya kuongeza nguvu chuoni hapo.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Machi 3, mwaka huu Kaimu Mkuu wa Chuo hicho, David Msuya amesema lengo la kuwahitaji madereva hao ni kwaajili ya kutoa mafunzo ya fani hiyo kwa wanafunzi wao.

“Tunaamini kwamba madereva ambao wamestaafu watakuwa na busara, ujuzi na maarifa makubwa katika kuwafundisha vijana wetu wanaokuja hapa chuoni kwa ajili ya mafunzo ya udereva na watakapomaliza mafunzo naamini watakuwa wameiva kwelikweli na wataweza kufanya kazi popote,” amesema.  

Ameongeza kuwa sifa nyingine ni vema dereva huyo awe na umri kuanzia miaka 60 na kuendelea na hata wale ambao waliacha kazi kwa sababu mbambali na kwa na uzoefu wa kutosha, asisite kupeleka maombi ya kazi katika chuo hicho.

Pia amesema wanaendelea kusajili wanafunzi kwa ajili ya kozi mpya ya Usomaji Mita za Maji ‘Water Meter’ na mwisho wa kupokea maombi ni Machi 17 mwaka huu.

Tofauti na hilo, Dkt Msuya amesema chuo chake kinahitaji walimu wa kujitolea kwa wanaoweza kufundisha kozi ya Bandari,  Biashara na zaidi walimu wake kike watapewa kipaumbele.

“Pia tunahitaji walimu wa masomo ya Hoteli, sifa awe na Diploma huyo tutampa makataba wa ajira hivyo wenye sifa tunawakaribisha,” amesema.

No comments:

Post a Comment