CHALAMILA AWAONDOA HOFU WAFANYABIASHARA KIPINDI HIKI CHA UCHAGUZI MKUU - MAGENDELA BLOG

Recent-Post

ads header

Friday, April 18, 2025

CHALAMILA AWAONDOA HOFU WAFANYABIASHARA KIPINDI HIKI CHA UCHAGUZI MKUU

NA MWANDISHI WETU

WAKATI joto la Uchaguzi Mkuu utakaofanyika nchini kote Oktoba mwaka huu likizidi kupanda wafanyabiashara jijini Dar es Salaam kutoka nje ya nchi wametakiwa kutokuwa na hofu kwani ulinzi na usalama wa mali zao umehimarishwa.

Hayo yamebainishwa leo jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila alipozungumza na waandishi wa habari na hakusita kupongeza mafanikio yanaendelea kupatikana kupitia maboresho ambayo yamefanywa na Mamlaka ya Bandari.

Amefafanua kuwa wanasiasa wengi wanakiri kuwa Serikali imefanya makubwa katika ujenzi wa miradi mbalimbali kupitia makusanyo ya ndani, hivyo kinachotakiwa sasa ni wananchi kuendelea kulipa kodi ili miradi mingine ya kimkakati ifanyiwe kazi ipasavyo.

"Kwa sasa tupo katika kipindi kinacholekea kwenye Uchaguzi Mkuu, hivyo inawezekana baadhi ya wafanyabiashara wakawa na hofu, ninachoweza kuwaambia wasiwe na hofu kwani Mkoa umejipanga kuhakikisha utulivu na amani inaendelea kutawala kabla na baada uchaguzi, "amesema.

Ameweka wazi kwamba hakuna taasisi, chama cha siasa, mashirika mbalimbali yatakayoweza kuvuruga amani iliyolindwa tangu zamani kutokana na misingi imara ya kiungozi hususan wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

 Ameongeza kuwa inawezekana ipo taasisi au makundi mengine yanaweza kuwa na malalamiko, hivyo kinachotakiwa ni kutumia haki zao za kimsingi vizuri kwa kufuata sheria nchi ili kuendelea kuifanya Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla kuwa na amani wakati wote.

Aidha amebainisha kuwa uongozi wa mkoa unafanya jitihada kadhaa ili kila mmoja asiwe na malalamiko katika kipindi hiki kinachoelekea kufanyika kwa uchaguzi mkuu na lengo ni moja tu, Dar es Salaam  na Tanzania iendelee kudumu katika misingi ya amani na utulivu.

 “Kwa sasa kama Mkoa tunasubiri taarifa ya Tume Huru ya Uchaguzi ili kupata taarifa kamili waliojitiandikisha na kusahihisha taarifa ili tuwezo kutoa ushirikiano wa kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu, niwaombe wafanyabishara wandelee na shughuli zao kama kawaida saa 24,” amesema.

Amefafanua kuwa baada ya kuzindua biashara kufanyika saa 24 hali inaendelea vizuri na mchakato ambao kwa sasa upo ni kwa wakuu wa Wilaya nao kujipanga katika maeneo yao ili wazindue biashara kufanyika saa 24 kama ambavyo mkoa imefanya.

Akizungumzia kuhusu Soko Kuu la Kariakoo, amebainisha kuwa limekamilika kwa asilimia 95 na wafanyabishara zaidi ya 1500 wameidhinisha na mchakato ambao unaendelea ni kuingia nao mikata kufanya shughuli zao hapo.

Pia amesisitiza mchakato mwingine ambao unaendelea ni kupitia madeni yote ya wafanyabishara ya nyuma kuhakikisha wanalipa kabla ya mchakato mwingine kuendelea.

“Naomba wakati michakato kadhaa ikiendelea viongozi wa wafanyabiashara kuhakikisha wanafungua njia ambazo zimezibwa na wafanyabishara wadogo bila shuruti ili kutoa nafasi kwa viongozi kupita kukagua asilimia zilizobaki hususan uzio ambao unaendelea kujengwa,” amesema

Akizungumzia mafanikio ambayo yamepatikana katika kipindi cha miaka minne, amesema anayojivua kwa sasa na kuwepo fungu kwaajili ya ujenzi ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa itakayojengwa kisasa kulingana na mahitaji yaliyopo.

Kuhusu ujenzi wa Daraja la Jangwani, amesema tayari mhandisi wa ujenzi ameshaanza kazi na anachofanya ni kujenga kambi za kuweka vifaa na ni dhahiri changamoto iliyokuwepo kwa kipindi kirefi inakwenda kuondoka, pindi daraja litakapokamilika.

 Chalamila pia ameongeza kuwa wananchi ambao waliondolewa eneo la kipawa, mchakato unaendelea wa kuhakikisha wananchi hao wanendelea kulipwa hatua kwa hatua na hakuna ambaye hatolipwa.


No comments:

Post a Comment