Sinach kuongoza jukwaa la Festival of Praise - MAGENDELA BLOG

Breaking

Recent-Post

ads header

Monday, October 3, 2022

Sinach kuongoza jukwaa la Festival of Praise

 


 

NA MAKUBURI ALLY

mally@tanzaniadaima.co.tz

MWIMBAJI mahiri wa nyimbo za Injili nchini Nigeria, Sinach Joseph Egbu anatarajia kuongoza jukwaa la Festival of Praise linalotarajia kufanyika Oktoba 16 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Tanzania Daima muandaaji wa tamasha hilo, mwimbaji maarufu hapa nchini, John Lissu alisema umahiri wa Sinach utafanikisha ujumbe wa neno la Mungu kuwafikia watanzania wote kupitia tungo zake na waimbaji wengine wa hapa nchini.

 Sinach - Wikipedia

Lissu alisema Sinach atapanda jukwaani na wimbo wake uliokamata anga la muziki wa Injili duniani wa ‘Way Maker’ uliotazamwa na mashabiki zaidi ya milioni 200.

Lissu alisema waimbaji wa hapa nchini watakaomsindikiza mwimbaji huyo ni pamoja Nay Eye, Christina Shusho, Ambwene Mwasongwe, Pasta EPA, Kwaya ya Kanisa la Moravian, Ruach Worship Team (Kenya) na Kwaya ya Gospel Winners.

Aidha Lissu alitoa wito kwa waamini wa muziki wa Injili kujitokeza kwa wingi kwenye tamasha hilo ambalo ni mojawapo ya matukio muhimu ya kusifu na kuabudu yanayofanyika hapa nchini.

mwisho          

No comments:

Post a Comment