Na. Majid Abdulkarim, WAF – Dar es Salaam
Wizara
ya Afya kupitia Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa
Hayapewi Kipaumbele (NTDS) imepanga kutoa Kingatiba kuthibiti Ugonjwa wa
matende na mabusha (Ngirimaji) kwa wakazi wapatao 4,449,499 kwa
halmashauri za Temeke, Kinondoni na Jiji la Dar es Salaam.
Hayo
yamebainishwa leo na Mratibu wa Magonjwa yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele
mkoa wa Dar es Salaam (RNTDS), Alex Mkamba ambapo amesema katika wakazi
hao wanatarajia kufikia mitaa 407 kati ya 535 na kata 70.
Mkamba
ameeleza wanatarajia kutoa elimu kwa watu 1,684 walimu wakiwa 330 na
watoa dawa 1354 katika halmashauri tatu za mkoa wa Dar es salaa ambazo
ni Temeke,Kinondoni na Jiji la Dar es Salaam.
“Kutokana
na utafiti ulofanyika hivi karibuni katika kupima maambukizi na vimelea
vya ugonjwa wa matende na mabusha kwa watoto wa darasa la kwanza na la
pili, katika mkoa wa Dar es salaam wilaya inayoongoza kwa maambukizi ni
Kinondoni kata ya Tandale 3.82%, Temeke kata ya Tandika 2.62% na
Jangwani 2.6”, amebainisha Mkamba
Mkamba
amesema mkoa wamejipanga kutoa elimu ya kutosha kwa kwa wananchi ili
kujenga uwezo wa kutambua ugonjwa unavyo ambukizwa na kuchukua tahadhali
kwa kufanya usafi wa mazingira na kutumia vizuri neti za kuzuia kuumwa
na mbu.
Pia Mkamba amehimiza wananchi matumizi sahihi ya dawa mara kwa mara pale panapobidi kumeza dawa hizo ili kupunguza maambukizi.
Naye
Afisa Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa Hayapewi
Kipaumbele (NTDS) kutoka Wizara ya Afya, Dkt. Clara Jones ameeleza
ugonjwa wa matende na mabusha ni hali ya kujaa maji sehemu za mwili kama
mikono, miguu, matiti na kwenye sehemu za siri kwa wanaume na wanawake.
“Ugonjwa
huu unasababishwa na minyoo inayoishi kwenye mfumo wa majidamu
inayojulikana kwa jina la kitaalum “Wuchereria bancrofti” unaoenezwa na
mbuu wa aina zote”, amesema Dkt. Clara
Kwa
upande wake Afisa Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa
Hayapewi Kipaumbele (NTDS) kutoka Wizara ya Afya, Oscar Kaitaba amesema
wamewajengea uwezo Waandishi wa Habari wa mkoa wa Dar Es Salaam kuhusu
ugawaji wa Kingatiba kuthibiti Ugonjwa wa matende na mabusha
(Ngirimaji).

No comments:
Post a Comment