Mkurugenzi wa Msama Promotion, Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), baada ya kufanya kikao na viongozi wa dini, Aprili 12, 2025 Mgahawa wa Food Point jijini Dar es Salaam cha kujadili maandalizi ya uzinduzi wa Tamasha la Kitaifa la kuombea uchaguzi mkuu. Kushoto ni Askofu Ndesario Mlaki kutoka makanisa ya Kipentekosti na kulia ni Mchungaji Mika Fanka wa Kanisa la Tanzania Assemblies Of God (TAG) la Beroya.
.......................................
NA DOTTO MWAIBALE
WACHUNGAJI
wa makanisa ya kiroho Mkoa wa Dar es Salaam wamesema maono ya Mkurugenzi wa
Kampuni ya Msama Promotion, Alex Msama ya kufanya matamasha ya kuombea uchaguzi
mkuu utakaofanyika mwezi oktoba mwaka huu ni ya muhimu kwa Taifa na yatachochoa
amani nchini.
Wakizungumza
kwa nyakati tofauti, maaskofu, wachungaji na mitume wa makanisa hayo katika
kikao cha maandalizi ya tamasha hilo kilichofanyika Mgahawa wa Food Point
jijini Dar es Salaam Aprili 12, 2025 kilichoandaliwa na Alex Msama walisema
maono hayo ya kimungu yana tija kubwa ni ya mhimu kwa Taifa.
Mchungaji
Mika Fanka wa Kanisa la Tanzania Assemblies Of God (TAG) la Beroya la Kipunguni
alisema maono hayo ya Alex Msama na uamuzi wa kuwashirikisha viongozi wa dini
kuliombea taifa wakati wa kipindi hiki muhimu cha uchaguzi ni ya kimungu na
yanapaswa kuungwa mkono na kila mtu hapa nchini.
“Sisi kama
kanisa na wawakilishi wa Mungu moja ya majukumu yetu ni kuliombea taifa na
viongozi wetu ili waweze kutuongoza kwa haki na tuwe na amani hivyo maono haya
makubwa ya Mkurugenzi Alex Msama kwa taifa letu tunampongeza sana na Mungu
akubariki,” alisema Mchungaji, Fanka.
Mchungaji Philipo Mdara wa Kanisa la Free Pentekoste Church Tanzania (FPCT), Gongolamboto Mwisho wa Lami alipongeza hatua hiyo ya Msama ya kuanzisha jambo hilo na kuwaweka pamoja viongozi wa dini ilikufanya maombi ya pamoja.
“Amani ya
Taifa lolote inatokana na maombi ya viongozi wa dini hivyo nimpongeze Msama kwa
jambo hili hivyo nichukue nafasi hii kuwaomba watanzania kujitokeza kwa wingi
eneo litakalopangwa kufanyika uzinduzi wa maombi hayo ya kitaifa yatakayoanzia
jijini Dar es Salaam,” alisema Mchungaji Mdara.
Kwa pande
wake Askofu Ndesario Mlaki kutoka makanisa ya Kipentekosti alisema Msama miaka
yote amekuwa akiandaa tamasha la Pasaka lakini kutokana na jambo kubwa la
kitaifa la uchaguzi mkuu Mungu
alimfunulia maono ya kuja na jambo hilo ili kipindi chote cha uchaguzi nchi iwe
na amani na utulivu.
Mchungaji
Rose David wa Kanisa la SWS Saa ya Wokovu ni Sasa aliwataka watanzania
kushiriki maombi hayo makubwa kama ilivyo kuwa wakati wa Corona hivyo ame
waomba wazee, vijana, wakina mama, baba na watoto kwenda kwenye uzinduzi wa
maombi hayo ya kitaifa.
Mkurugenzi
wa Msama Promotion, Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari baada ya
kufanya kikao na viongozi hao wa dini alisema uzinduzi wa tamasha hilo
utafanyika Juni 21, 2025 jijini Dar es Salaam na kuwa wanafanya mchakato wa
kuona watafanyia wapi lakini kutokana na umuhimu wake na kuwa ni jambo la kitaifa
wanaendelea kuomba lifanyike Uwanja wa Uhuru au wa Benjamin Mkapa kwani bado
hawajapata majibu kutokana na viwanja hivyo kuwa katika ukarabati.
Alisema
maandalizi ya tamasha hilo yanaendelea vizuri na kuwa siku hiyo ya uzinduzi
kutakuwa na wanamuziki kutoka mataifa mbalimbali kama Afrika Kusini, Zambia,
Nigeria, Rwanda, Congo, Uganda na Kenya kwa ajili ya kutoa burudani.
“ Mchakato
tunaoendelea nao hivi sasa ni pamoja na kumpata mgeni rasmi ambaye atakuwa wa
ngazi ya juu pamoja na kuwaomba wadhamini wa kutu sapoti kwani tamasha hili
litakuwa na mahitaji makubwa ya fedha kwa ajili ya kuwaleta wanamziki hao ambao
watahitaji chakula, malazi, usafiri na kuwalipia wanapoingia nchini,” alisema
Msama.
Mchungaji Philipo Mdara wa Kanisa la Free Pentekoste Church Tanzania (FPCT), akizungumza kwenye mkutano huo.
Mchungaji Mika Fanka wa Kanisa la Tanzania Assemblies Of God (TAG) la Beroya la Kipunguni, akizungumza.
Mchungaji, Alex Kishimba, akisisitiza jambo katika mkutano huo.
Viongozi wa dini kutoka makanisa ya kiroho wakiwa kwenye kikao hicho.
Kikao hicho kikiendelea.
Mkurugenzi wa Msama Promotion, Alex Msama (wa tatu kutoka kulia), akiwa na viongozi wa dini wakati akizungmza na waandishi wa habari.
No comments:
Post a Comment